Raia wa Tanzania wanauomboleza aliyekuwa rais wa Tanzania John Pombe Magufuli lakini kwa wakazi wa Chato ni zaidi ya hilo kwasababu hii ndio itakuwa mara ya mwisho kumuona mwana wao .
Ikilinganishwa na
awali ambapo alisimama kandokando ya barabara ili kuwahutubia , wakati huu
hatozungumza kwa makumi ya maelfu ambao watamsubiri kandokando ya barabara
inayoelekea nyumbani kwake huko Chato.
Hii Leo mwili wa
kiongozi huyo wa Tanzania utazikwa huku maelfu ya raia wa taifa la Tanzania
wakisubiri kuhudhuria mazishi yake.
Rais Magufuli
alifariki kutokana na maradhi ya moyo wakati alipokuwa akipatiwa matibabu
katika hospitali ya Mzena jijini Dar es
Salaam tarehe 17 Machi.
Hii ni mara ya kwanza
kwamba Watanzania kumzika rais aliyefariki akiwa madarakani katika miaka 60 ya Uhuru.
Kama inavyotarajiwa ,
taifa hilo limekuwa likikumbwa na huzunitangu kifo chake kilipotangazwa na makamu wake usiku wa tarehe 17 mwezi
Machi.
Hii leo Misa mbili maalum
zitafanyika. Ya kwanza ikifanyika katika kanisa ambalo alikuwa akienda kufanya
ibadaChatona misa ya pili ikifanyika katika uwanja wa
Mgufuli , ambapo maelfu ya waombolezaji wamekongamana.
Kutoka hapo atazikwa
katika makaburi ya familia chini ya itifaki zote za kumzika amiri jeshi mkuu.
Bwana Magufuli atakumbukwa kwa kuwa mkatoliki mkakamavu ,
atakumbukwa na wengi kwa vita vyake dhidi ya ufisadi, na ujenzi wa miradi
mikubwa ya maendeleo.
Hili lilishuhudiwa siku ya
Jumatatu wakati viongozi kadhaa wa Afrika walipomuenzi katika mazishi ya
kitaifa yaliofanyika katika mji mkuu wa Dodoma.
Kwengineko pia atakumbukwa
kama kiongozi ambaye hakuvumilia wapinzani wake wa kisiasa , alikandamiza
vyombo vya habari na wanaharakati.
Pia atakumbukwa kwa jinsi
alivyokabiliana na mlipuko wa virusi vya corona.