Kifo cha Rais Magufuli: Wanyarwanda wako pamoja na Tanzania wakati huu mgumu

Dunia yaomboleza kifo cha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli.

Moja kwa moja

Asha Juma and Dinah Gahamanyi

  1. Kifo cha Rais Magufuli: Rais wa Venezuela amuomboleza Magufuli

    Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, ametuma salamu za rambi rambi kwa Watu wa Tanzania kufuatia kifo cha Rais John Magufuli.

    Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya nje imesema "tunasimama" na "ndugu zetu wa Tanzania".

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

  2. Kifo cha Rais Magufuli: Je, Katiba ya Tanzania inatoa mwongozo gani anapofariki Rais?

    Rais Magufuli alishinda uchaguzi kwa mara ya pili mwezi Oktoba mwaka jana

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Rais Magufuli alishinda uchaguzi kwa mara ya pili mwezi Oktoba mwaka jana

    Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amefariki dunia Jumatano jioni; na swali la wengi ndani na nje ya Tanzania kwa sasa ni nini kitakachofuata kwa mujibu wa Katiba?

  3. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli:Balozi wa Marekani atuma salamu za rambirambi kwa Watanzania

    Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright ametuma salamu za rambirambi kwa Watanzania kupitia ukurasa wake wa Twitter; "Kwa niaba ya watu wa Marekani, Ninatuma salamu zangu za rambirambi kwa kila mmoja anayeomboleza kifo cha Rais Magufuli hii leo.

    Ifahamike kuwa Marekani iko pamoja na Watanzania katika wakati huu mgumu".

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

  4. Habari za hivi punde, Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Watanzania waomboleza kifo cha Magufuli

    Maelezo ya video, Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Watanzania wamuomboleza rais wao
  5. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: 'Nikifa nizikwe nyumbani kule alikozikwa baba ''Chato''

    Rais John Pombe Magufuli
  6. Raila Odinga amuomboleza rafiki yake rais Magufuli

    Raila Odinga

    Aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya na kiongozi wa upinzani Raila Odinga ametuma risala za rambirambi kwa familia ya rais John Pombe Magufuli na raia wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

    Katika taarifa kwa vyombo vya habari Raila amemtaja marehemu kama kiongozi aliyejaribu kuimarisha hali ya raia wa Tanzania.

    Amesema kwamba rais Magufuli amekuwa rafiki yake wa muda mrefu na kwamba amekuwa kando yake wakati mgumu alipomuhitaji.

    Amesema kwamba tangazo la kifo chake amelipokea na huzumi kubwa akiongezea kwamba anasimama na familia ya marehemu wakati huu wa maombolezo.

    Kiongozi huyo amesema kwamba kwa miaka kadhaa iliopita ameshirikiana na rais Magufuli haswa katika kuiunganisha Afrika mashariki kupitia miundo msingi.

    Amewataka Watanzania wote kusalia watulivu na kufuata utamaduni uliowachwa na rais wa kwanza wa taifa hilo Julius Nyerere na wa viongozi waliofuata katika kukabidhiana mamlaka kulingana na katiba ya taifa hilo

  7. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Tarehe za matukio Muhimu katika maisha ya Rais John Pombe Magufuli

    Magufuli

    Chanzo cha picha, Getty Images

    • 1959- Azaliwa Chato kaskazini magharibi mwa Tanzania
    • 1995- Achaguliwa kuwa mbunge kwa mara ya kwanza
    • 2000- Ateuliwa kuwa Waziri
    • 2015- Achaguliwa kuwa rais kwa muhula wake wa kwanza
    • 2020- Achaguliwa kwa kipindi cha pili kuwa rais
    • 2020 Novemba tarehe 5 – Aapishwa kwa muhula wa Pili
    • 2021 Machi Tarehe 7- Uvumi unaanza kuenea kuhusu aliko rais Magufuli baada ya kukosa kuonekana kwa muda wa wiki moja
    • 2021 Machi tarehe 11 – Vyama mbali mbali vya Upinzani nchini Tanzania vyataka kujua hali ya rais Magufuli na aliko
    • 2021 Machi Tarehe 12 -Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akana kwamba rais Magufuli anaugua asema yupo ‘ buheri wa afya na anaendelea kuchapa kazi’
    • 2021 Machi Tarehe 15 – Makamu wa Rais Samia Suluhu awapa Watanzania ‘salamu’ kutoka kwa Rais Magufuli huku hofu ikizidi kuhusu hali yake na aliko
    • 2021 Machi, tarehe 6 - Alazwa katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete kwa tatizo la moyo la mfumo wa umeme
    • 2021 Machi tarehe 7 - Aliruhusiwa kurejea kazini
    • 2021 Machi tarehe 14 - Alikimbizwa Hospitali ya Mzena Dar es Salaam kuendelea na matibabu
    • 2021 Machi tarehe 17 saa kumi na mbili jioni - Magufuli afariki dunia
    • 2021 Machi tarehe 17 Usiku – Makamu wa rais Samia Suluhu atangaza kupitia runinga kifo cha rais Magufuli .Siku 14 za maombolezo zatangazwa.Bendera kupeperushwa nusu mlingoti.
  8. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Buriani Rais John Pombe Magufuli

    Rais John Pombe Magufuli
  9. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Risala za rambirambi kutoka kwa viongozi mbalimbali Tanzania

    Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania Fredrick Sumaye

    Kufuatia kifo cha Rais John Magufuli wa Tanzania watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa na serikali wamelezea hisia zao na namna walivyopokea taarifa za kifo cha kiongozi huyo, ambaye ni Rais wa awamu ya tano wa taifa hilo.

    Miongoni mwao ni Waziri mkuu wa zamani wa taifa hilo Fredrick Sumaye, ambaye wakati huo akiwa waziri mkuu, Rais Magufuli alikuwa kwenye nafasi ya naibu waziri na baadaye waziri katika wizara ya Ujenzi.

    Sumaye anaeleza alivyopokea taarifa hii ya msiba huu,

    ‘’Mimi niliziona taarifa hizi kwenye runinga nikashutuka kama sio kitu cha kweli, na mwanzoni watu walionipigia simu nilisema siamini kama ni za kweli, lakini sasa naamini ni za kweli. Ni taarifa imetushutusha sana, ni taarifa imetusikitisha sana kama taifa, kwasababu taifa kupoteza rais ambaye yuko kwenye kiti siyo jambo dogo. Rais Magufuli wote tunamjua ni mchapa kazi, ni msema kweli na lile alaolisema ndilo analotenda. Tumesikitika sana kumpoteza kiongozi wetu huyu, Rais wetu mpendwa lakini ndio kazi ya Mungu.’’

    Mheshimiwa Sumaye amekuwa kwenye serikali kwa kipindi cha zaidi ya miaka 25 na amehudumu kama waziri mkuu na amemtaja Rais Magufuli kama mtu ambaye haogopi kufanya maamuzi.

    Zitto Kabwe

    ‘’Nimepokea taarifa za msiba wa Rais Magufuli kwa masikito makubwa, nimemuona makamu rais akitangaza msiba huu na vilevile nimempigia simu ya kumpa pole kwasababu sasa kwa mujibu wa katiba yetu yeye ndio rais mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya muda mfupi atakula kiapo cha kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni majukumu mazito sana kwake na pia msiba huu ni mkubwa sana. Kwa niaba ya chama cha ACT- Wazalendo na kwa niaba yangu binafsi, natoa pole kwa mama yetu Janet Magufuli na familia nzima ya hayati John Pombe Joseph Magufuli, tuko pamoja nao katika kipindi hiki kigumu. Natuma salamu zangu pia za rambirambi kwa makamu mwenyekiti wa CCM na wanachama wa CCM kwa kuondokewa na mwenyekiti wao wa taifa’’.

    Bwana Zitto Kabwe amemzungumzia Bwana Magufuli ambaye amekuwa kiongozi wa nchi yao katika nyadhifa mbalimbali na ‘’kwa hakika alitekeleza wajibu wake kwa juhudi kubwa. Taifa litamkumbuka kwa mchango wake kwenye maendeleo yetu’’.

    Fatma Karume

    Chanzo cha picha, FATMA KARUME/FACEBOOK

    Fatma Karume, mwana wa Abeid Karume naye pia amezungumza na BBC na kutoa risala zake.

    ‘’Inasikitisha sana imechukua muda mrefu kwa wananchi kuambiwa ukweli, Kwa muda mrefu nchi ilikuwa kwenye taharuki. Lakini Mungu mlaze mahala anapostahiki kumlaza’’. Fatuma Karume amemuelezea kama rais wa nchi hana uhakika kama atakumbukwa na watu wengi kwa mema kwa maana kwamba tangu alipoingia kwenye urais, nchi ya Tanzania imebadilika sana, imekuwa nchi ya huzuni, akidai kuwa uhuru wao binafsi umechukuliwa. ‘’Naomba tuache kuumizana, turudi kwenye upendo’’.

  10. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amuomboleza Rais Magufuli

    Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson ameelezea kusikitishwa na kifo cha rais wa Tanzania John Pombe Magufuli Amekuwa miongoni mwa viongozi wa kwanza duniani kutuma salamu za rambi rambi baada ya kutangazwa kwa kifo cha Magufuli . '‘ Fikra zangu zipo na wapendwa wake pamoja na Watanzania’amesema kupitia ujumbe aliondika kwenye twitter.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Kulingana na katiba ya Tanzania makamu wa rais wa nchi hiyo Samia Hassan Suluhu ataapishwa kuhudumu kama rais mpya ili kukamilisha muda uliosalia wa muhula wa miaka mitano wa Magufuli ulioanza mwaka jana''.

  11. Kifo cha Rais John Pombe Magufuli: Mkuu wa WHO amuomboleza Magufuli

    Magufuli

    Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani (WHO) Tedros Adhanom ametuma salamu za rambirambi kwa Watanzania na serikali ya nchi hiyo kufuatia kifo cha Rais John Pombe Magufuli.Kupitia ujumbe wa Twitter Teodros amesema Shirika hilo limewaweka Watanzania pamoja na familia ya rais Magufuli wakati huu mgumu:

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

  12. Hujambo na Karibu kwa matangazo haya maalumu ya moja kwa moja kuhusu kifo cha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli