Wanawake 15 na watoto sita waliokuwa wametekwa na wanamgambo wa
Islamic State katika jimbo lenye utajiri wa mafuta la Cabo Delgado nchini
Msumbiji wameokolewa na jeshi.
Wengi
wao walikuwa wametekwa kutoka katika kisiwa cha Matemo wiki iliyopita, kulingana na mkuu wa polisi Bernardino Rafael.
Mapigano
ya hivi karibuni yanaonesha kua vikosi vya usalama vilifahamu ni wapi walipokuwa
wanamgambo hao, kwa hiyo kwa usaidizi wa helikopta waliweza kuwazingira na
kuwatenganisha na watekaji wao, alisema.
Watarejeshwa tena Matemo, eneo ambalo limezongwa na mashambulizi tangu mwezi Oktoba.
Lakini mkuu wa polisi amesema kuwa kisiwa
hicho ni salama kwa sasa.
Wanamgambo wa IS, wanaofahamika na wakazi kama al-Shabab,
au vijana , wamefanya mashambulio kadhaa katika vijiji na miji katika eneo hilo
kwa zaidi ya miaka mitatu.
Hivi karibuni zaidi
waliahidi kulitii kundi la IS , na wanafahamika kwa mashambulio ya ukatili,
ambayo huwa ni pamoja na kuwakata vichwa wanavijiji na kuchoma moto nyumba.
Mara nyingi huwateka
wanawake na watoto ambao hutumiwa kama watumwa wa ngono na kusafirisha bidhaa
walizoiba kufuatia mashambulio.
Mwishoni mwa juma,
Waziri wa ulinzi wa Marekani alisema kuwa Anthony Tata, naibu waziri wa mashauri
ya kigeni anayehusika na masuala ya sera alitembelea Msumbiji Ijumaa na kufanya
mazungumzo na mawaziri juu ya umuhimu wa mpango wa kimkakati wa kuleta utulivu
katika jimbo la Cabo Delgado.
Taarifa
kutoka ubalozi wa Marekani inasema kuwa Marekani itatoa msaada wa kibinadamu na
kiuchumi wa dola milioni 42 kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika jimbo hilo
lililopo kaskazini mwa nchi.
Juhudi hizi na nyinginezo, kwa mujibu wa balozi Dennis
Hearne, ni sehemu ya msaada wa kila mwaka wa dola milioni 500 ambao Marekani
hutoa kwa Msumbiji.