Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Zitto Kabwe: 'Nitampigia Kura Tundu Lissu awe rais wa Tanzania'

Kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT-wazalendo, Zitto Kabwe ametoa tamko kuwa kura yake itaenda kwa mgombea wa chama cha upinzani cha Chadema.

Moja kwa moja

Dinah Gahamanyi

  1. Na mpaka hapo ndio tunafikia mwisho wa matangazo yetu ya moja kwa moja kwa leo. Tukutane tena Jumatatu 19.10.2020

  2. Zitto Kabwe: 'Nitampigia Kura Tundu Lissu awe rais wa Tanzania'

    Kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT-wazalendo, Zitto Kabwe ametoa tamko kuwa kura yake itaenda kwa mgombea wa chama cha upinzani cha Chadema.

    Anasema kamati ya Uongozi ya Chama chake cha ACT imeshauriana na kuona kuwa huu ni mwaka wa kihistoria kwa Watanzania, mwaka wa kuamua hatma ya Maisha yao.

    "Kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mimi Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe nitampigia kura kwa ndugu Tundu Antipas Mughwai Lissu. Huyu ndiye Mgombea wa Upinzani ambaye ana nguvu ya kumshinda mgombea wa chama tawala."

    Anasema hatua hii ya kumuunga mkono mgombea wa chama kingine imesukumwa na dhamira yake ya kuleta mabadiliko ya kumchagua Lissu.

    Kabwe ameyaeleza hayo katika hotuba yake ya kampeni Bangwe, Kigoma na kuwataka wafuasi wa chama hicho pia kumpigia kura Lissu.

    Mwezi Septemba Mwenyekiti wa ACT Maalim Seif Shariff Hamad, alitangaza kumuunga mkono Lissu kwenye kinyang'anyiro cha Urais.

    ACT katika kinyang'anyiro cha urais imemsimamisha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Benard Membe, ambaye mpaka sasa hajajitokeza hadharani kumuunga mkono Lissu.

    Mara baada ya Maalim Seif kutangaza kumuunga mkono Lissu, Mmembe alisisitiza kuwa yeye ndiye mgombea halali wa ACT.

    Chadema kwa upande mwengine kimetangaza kumuunga mkono Maalim kwenye kinyang'anyiro cha urais wa Zanzibar.

    Hata hivyo, ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa vimeoynya juu ya ushirikiano wa vyama hivyo ikisema ni kinyume na sheria.

    Soma zaidi:

  3. Polisi akamatwa kwa kuwashambulia waandamanaji Nigeria

  4. Wakulima waadhimisha siku ya chakula Tanzania

  5. Yanga yamkaribisha Tanzania kocha Mrundi

  6. Rusesabagina 'ameandika barua' kutoka jela

  7. Africa ‘haiwezi kuhimili’ wimbi la pili la virusi vya corona

  8. Maalim asimamishwa kufanya kampeni za urais Zanzibar

      • Author, Aboubakar Famau
      • Nafasi, BBC News, Dar es Salaam