Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Zitto Kabwe: 'Nitampigia Kura Tundu Lissu awe rais wa Tanzania'
Kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT-wazalendo, Zitto Kabwe ametoa tamko kuwa kura yake itaenda kwa mgombea wa chama cha upinzani cha Chadema.
Moja kwa moja
Dinah Gahamanyi
Zitto Kabwe: 'Nitampigia Kura Tundu Lissu awe rais wa Tanzania'
Kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT-wazalendo, Zitto Kabwe ametoa tamko kuwa kura yake itaenda kwa mgombea wa chama cha upinzani cha Chadema.
Anasema kamati ya Uongozi ya Chama chake cha ACT imeshauriana na kuona kuwa huu ni mwaka wa kihistoria kwa Watanzania, mwaka wa kuamua hatma ya Maisha yao.
"Kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mimi Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe nitampigia kura kwa ndugu Tundu Antipas Mughwai Lissu. Huyu ndiye Mgombea wa Upinzani ambaye ana nguvu ya kumshinda mgombea wa chama tawala."
Anasema hatua hii ya kumuunga mkono mgombea wa chama kingine imesukumwa na dhamira yake ya kuleta mabadiliko ya kumchagua Lissu.
Kabwe ameyaeleza hayo katika hotuba yake ya kampeni Bangwe, Kigoma na kuwataka wafuasi wa chama hicho pia kumpigia kura Lissu.
Mwezi Septemba Mwenyekiti wa ACT Maalim Seif Shariff Hamad, alitangaza kumuunga mkono Lissu kwenye kinyang'anyiro cha Urais.
ACT katika kinyang'anyiro cha urais imemsimamisha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Benard Membe, ambaye mpaka sasa hajajitokeza hadharani kumuunga mkono Lissu.
Mara baada ya Maalim Seif kutangaza kumuunga mkono Lissu, Mmembe alisisitiza kuwa yeye ndiye mgombea halali wa ACT.
Chadema kwa upande mwengine kimetangaza kumuunga mkono Maalim kwenye kinyang'anyiro cha urais wa Zanzibar.
Hata hivyo, ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa vimeoynya juu ya ushirikiano wa vyama hivyo ikisema ni kinyume na sheria.
Soma zaidi:
Kawaida maji ya juu ya ziwa yakiwa baridi - kwasababu ya hali joto ya baridi au mito inayobeba theluji iliyoyeyuka, kwa mfano, - maji hayo baridi ambayo ni mazito huzama na yale ambayo sio mazito hupanda juu ya ziwa. Bofya kiunganishi hiki kusoma taarifa hii zaidi..https://bbc.com.im/swahili/54568727%3C/a%3E%3C/p%3E%3C/div%3E%3C/div%3E%3C/article%3E%3C/li%3E%3Cli class="css-xxlek1">
Mfanyabiashara haramu ya binadamu akamatwa Libya
Polisi akamatwa kwa kuwashambulia waandamanaji Nigeria
Wakulima waadhimisha siku ya chakula Tanzania
Yanga yamkaribisha Tanzania kocha Mrundi
Rusesabagina 'ameandika barua' kutoka jela
Africa ‘haiwezi kuhimili’ wimbi la pili la virusi vya corona
Maalim asimamishwa kufanya kampeni za urais Zanzibar
Maelezo kuhusu taarifa - Author, Aboubakar Famau
- Nafasi, BBC News, Dar es Salaam
Hujambo na karibu kwa matangazo yetu mubashara leo Ijumaa tarehe 16.10.2020