Huenda Kenya
ikaanza kujaribu kuwatibu wagonjwa wa Covid-19 kwa kutumia plasma. Plasma ni sehemu ya maji maji ya damu ambayo inabakia
wakati seli zote nyeupe na nyekundu za damu pamoja na ute mweupe vinapoondolewa.
Dokta Mercy Mwangangi kutoka
Wizara ya Afya anasema kuwa watalaam wanandaa miongozo ambayo itawaruhusu madakatari
kutumia sehemu hii ya damu kama tiba ya corona.
'Katika uchunguzi huu,
watalaam, watakuwa wanachunguza uwezekano wa kuchukua damu ya mtu ambaye
amepona baada ya kuambukizwa corona na kuitumia damu hiyo kumtibu yeyote ambaye
amepatikana na maambukizi hayo,” Dokta Mwangagi aliwaelezea wanahabari.
Mbinu hiyo ya kutumia damu
kumtibu mtu mwingine ni matibabu ya kale.
Dawa hii inapunguza uvimbe wa mwili kulingana na homoni
inayotengenezwa ndani ya mwili. Katika janga hili, dawa hili hutumika kwa wale ambao wako
katika hali mahututi na hawawezi kupuma vizuri.
Plasma inatumiwa kwasababu ina kinga ya mwili. Lakini, kwa
sasa wataalam hawajui kinga hiyo inadumu kwa muda ngapi au siku ngapi.
Kuna zaidi ya majaribio 80
ambayo yanalenga kuwasajili wagonjwa kushiriki katika uchunguzi huu kote
duniani.