Miili 53 yazikwa katika makaburi ya pamoja Morogoro Tanzania
Watu 71 wamethibitishwa kufariki dunia na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa baada ya lori la mafuta kulipuka katika eneo la Msamvu mjini Morogogoro, Mashariki mwa Tanzania.
Moja kwa moja
Habari za hivi punde, Waliothiriwa wazungumza na BBC
Maelezo ya video, Jamaa za walioathiriwa wawatafuta wapendwa wao
Wakazi waliojawa na hofu huenda wamepoteza wapendwa wao wamekusanyika katika hospitali ya Rufaa ya Morogoro kujulia hatma ya wapendwa wao.
Habari zaidi zinasema kuwa jamaa hao wameombwa kuondoka hospitali hapo na kurejea kesho kwa maelezo zaidi.
Habari za hivi punde, Baadhi ya majeruhi wapelekwa Muhimbili
Maelezo ya picha, Manusura wa mkasa wa Morogoro
Miili ya watu 60 ajali ya lori la mafuta Morogoro imehifadhiwa mochwari
Maelezo ya picha, Wazima moto walikuwa na wakati mgumu kukabiliana na moto huo
Mkuu
wa Mkoa
Morogoro, Dk
Stephen Kebwe
amesema miili ya watu 60 waliokufa baada ya lori la mafuta
kupinduka eneo la Msamvu mkoani Morogoro na kuwaka moto
muda mfupi baada ya watu kuanza kuchota mafuta hayo
imehifadhiwa mochwari.
Akizungumza Gazeti la Mwananchi Dk Kebwe
amesema zaidi ya watu 70 wamejeruhiwa na kupelekwa
Hospitali ya Mkoa huo wa matibabu.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Dk Ritha
Lyamuya amesema walipokea miili 60 kufikia leo saa 5:30
asubuhi na kwamba bado wanaendelea kupokea mingine.
“Majeruhi tuliowapokea hapa 52 wanaume na wanane ni
wanawake. Tumelazimika kuwaomba madaktari na wauguzi
kutoka hospitali na vituo vingine vya afya katika manispaa ya
Morogoro kwa kuwa leo ni mapumziko,” amesema Lyamuya.
Tanzania yaomboleza
Maelezo ya picha, Ishara ya maombolezo
Watu kutoka kila pembe ya Tanzania wamekuwa wakituma risala za rambi rabi kufuatia mkasa wa moto wa lori la mafuta lililolipuka mjini Morogoro Mashariki mwa Tanzania.
Wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii ya kuwafariji wale wote waliofikwa na msiba.
Wito unazidi kutole wa watumiaji wa mitandao hiyo wakome kusambaza picha ya miili ya watu iliyoteketea vibaya.
Habari za hivi punde, Hali ilivyo katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro
Maelezo kuhusu taarifa
Author, Aboubakar Famau
Nafasi, BBC Africa, Morogoro
Maelezo ya picha, Walioathiriwa
Baadhi ya waathiwa wa mkasa wa Morogoro ambao wako katika pilka pilka za kuwatafuta wapendwa wao ambao huenda wamehusika katika ajali ya lori la mafuta wamezungumza na mwandishi wa BBC Aboubakar Famau ambaye kwa sasa yuko katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro
Jamaa za walioathiriwa wawatafuta wapendwa wao
Maelezo ya picha, Jamaa za walioathiriwa
Mwandishi wa BBC Aboubakar Famau ambaye yuko katika eneo la tukou anaripoti kuwa wakazi walio na hofu huenda wamepoteza wapendwa wao wamekusanyika karibu na eneo la tukio kujulia hatma ya wapendwa wao.
''Nimempigia ndugu yangu simu ambaye ni mwendesha piki piki lakin hapokei simu'' alisema mmoja wao
Muda mfupi baada ya Lori la mafuta kushika moto Morogoro
Si mara ya kwanza visa vya moto inayotokana na malori yaliobeba shehena ya mafuta kutokea katika enao la Afrika Mashariki na Kati.
Mwaka 2010 watu 292 walifariki dunia nchini Jamhuri ya Kidemocrasia ya na miaka mitano baadae watu 203 wakafarikiki nchini Sudan Kusini.
Maelezo ya picha, Mkaazi wa Morogoro atazama kwa mshangao moto huo
Nini kilichotokea Morogoro?
Maelezo ya picha, Pikipiki zilizoteketa
Mmoja wa manusura wa mkasa huo alisikika akisimulia kilichojiri.
"Hapa nilikuta watu wanang'ang'ania mafuta na watu walikuwa bizee kuchota mafuta na hawaelewi haya ni mafuta au maji. Katika huo mshangao sasa mimi nasikia moto umelipuka. Moto ulipozuka tukaanza kukimbiana, kila mmoja anajiokoa kivyake vyake, kufikia hapo nimeanguka chini nikaanza kutambaa kwa magoti nikufanikiwa kuondoka ." alisema manusura huyo
Walioshuhudia ajali hiyo wanasema waendesha piki piki ndio walioathirika zaidi na mkasa huo.
Uchunguzi kuhusiana na ajali hiyo umeaanza
Maelezo ya picha, Ramani ya Tazania
Watu 60 wamethibitishwa kufariki na wengine zaidi ya 65 kujeruhiwa baada ya lori la mafuta kulipuka katika eneo la Msamvu mjini Morogoro, Mashariki mwa Tanzania.
Polisi wanasema watu hao walikuwa wakichota mafuta baada ya lori hilo kupinduka katika bara bara kuu mapema Jumamosi wakati ajali hiyo ilipotokea.
Bado chanzo cha ajali hiyo hakijathibitishwa lakini kuna hofu huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka.
Tamko la Rais Magufuli kuhusu ajali ya lori la mafuta Tanzania
Chanzo cha picha, Ikulu Tanzania
Maelezo ya picha, Rais wa Tanzania John Magufuli
Rais wa Tanzania, John Magufuli amepokea amesema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watu zaidi ya 60 na wengine 70 kujeruhiwa vibaya baada yakuungua kwa moto baada ya lori lililokuwa na shehena ya mafuta kupata ajali na kisha kulipuka moto Mjini Morogoro.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania, Gerson Msigwa imesema Rais Magufuli ametoa pole kwa familia, ndugu, marafiki na wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hiyo na pia amewaombea majeruhi wapone haraka.
Taarifa hiyo pia imekemea vitendo vya wananchi wanaovamia magari yenye milipuko akitaka vikomeshwe mara moja.
Ajali hiyo ilitokea mapema Jumamosi mwendo wa saa mbili asubuhi wakati ambapo lori hilo lililokuwa linatoka Dar es Salaam limepinduka karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu baada ya dereva
wa lori kumkwepa mwendesha pikipiki na kisha mafuta yaliyokuwa yakimwagika kushika moto na kuunguza watu waliokuwa wanayachota.
"Nimeumia sana kusikia idadi kubwa ya Watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali hii, natoa pole kwa wote walioguswa na vifo hivi hasa familia za marehemu wote, nawaombea marehemu wapumzike mahali pema peponi na majeruhi wote wapone haraka" amesema Rais Magufuli.