CAF lathibitisha kifo cha Hussein Swaleh Mtetu
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetoa taarifa rasmi kuhusu kufariki kwa aliyekuwa katibu mkuu wa shirikisho la taifa na afisa mkuu wa soka Kenya, Hussein Swaleh Mtetu ambaye alikuwa miongoni mwa Wakenya 32 waliofariki.
Inaarifiwa Hussein Swaleh alikuwa anarudi nyumbani baada ya kuhudumu kama kamishna katika ligi ya mabingwa ya CAF katika mechi kati ya Ismaily SC (Misri) na TP Mazembe (Jamhuri ya Kidmeokrasi ya Congo) iliyochezwa Ijumaa huko Alexandria.