Mwandishi wa BBC Thomas Fessy aliye mjini Banjul anasema maandalizi ya kuwalaki marais wa Guinea na Mauritania uwanja wa ndege, Alpha Conde na Mohamed Ould Abdel Aziz.
Wanajeshi uwanjani wanatabasamu na kuonesha urafiki.
Mjumbe wa UN Afrika Magharibi Mohamed Ibn Chambas ambaye amemtaka Jammeh kung’atuka tayari amewasili.
Jijini, kimya kimetanda na biashara nyingi zimefungwa.
Wengi wanaamini mwisho wa mzozo wa sasa wa kisiasa unakaribia lakini wanasubiri Jammeh atawaambiaje marais hao wanaofika kumshawishi kuondoka kwa Amani.
Mwenyekiti wa tume ya Ecowas, Marcel de Souza, amependekeza Jammeh apelekwe Guinea kabla ya hatima yake kuamuliwa.
Mauritania si mwanachama wa Ecowas.
Rais wa Guinea Alpha Conde amekuwa akipinga pendekezo la majeshi kutumia kumuondoa Jammeh. Anasema diplomasia inafaa kutumiwa.