Wamarekani saba wawekwa karantini katika kituo cha Ebola nchini Kenya

Chanzo cha picha, Getty Images
Wafanyakazi saba wa misaada kutoka Marekani, ambao walikuwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kusaidia juhudi za kukabiliana na mlipuko wa Ebola, wamewekwa karantini nchini Kenya baada ya serikali ya Marekani kuweka masharti mapya ya usafiri kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters na mkuu wa shirika la misaada la Marekani lililowaajiri.
Wafanyakazi hao wa misaada ni wa kwanza kuwekwa karantini katika kituo hicho, ambacho ujenzi wake ulipingwa vikali nchini Kenya na kesi dhidi yake inaendelea mahakamani, baada ya jaji kuamuru shughuli katika za kuistishwa hadi uamuzi utakapotolewa.
Licha ya agizo hilo la mahakama kituo hicho kimeendelea na shughuli zake, kulingana na maafisa wa Marekani na picha za satelaiti zilizochunguzwa na Reuters.
Sera mpya ya Washington inaeleza kuwa raia wa Marekani wanaorejea kutoka DR Congo, ambako kuna mlipuko wa Ebola, lazima wakae kwa wiki tatu katika nchi ya tatu kabla ya kuingia Marekani.
Mwezi uliopita, Waziri wa Afya wa Kenya Adan Duale alitangaza kusimamishwa mara moja kwa ujenzi wa kituo hicho baada ya serikali kupatikana na hatia ya kupuuza mahakama kwa kushindwa kutii amri za kusimamisha ujenzi wa kituo hicho cha karantini.
Unaweza kusoma:



























