Mshauri wa spika wa Iran:Trump na Netanyahu wanakutana kujadili kushambulia Iran, sio mazungumzo
Wakati huo huo, Mshauri wa spika wa bunge la Iran anasema kuwa mada ya mkutano wa wiki hii kati ya Waziri Mkuu wa Israel na Rais wa Marekani itakuwa ni shambulizi dhidi ya Iran.
Mehdi Mohammadi aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa X: "Trump na Netanyahu watajadili "operesheni" na sio mazungumzo." Mshauri wa kimkakati Mohammad Baqer Qalibaf aliongeza kuwa "hakuna utata kuhusu hili."
Ofisi ya Benjamin Netanyahu ilitangaza kwamba anapanga kukutana na Donald Trump huko Washington Jumatano ili kujadili mazungumzo na Iran.
Wawakilishi wa Iran na Marekani walikutana tena mjini Muscat Ijumaa iliyopita, na upatanishi wa Oman, baada ya mapumziko ya miezi kadhaa.
Awali Israel ilisema kuwa haina haja ya kufanya mazungumzo na utawala wa sasa wa Iran kwani nchi jirani zinataka mabadiliko ya uongozi.
Soma pia: