Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Marekani yasubiri jibu la Iran kuhusu mapendekezo ya kusitisha mapigano - Rubio

Kauli hiyo imejiri baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, kusema kila jitihada za kutafuta suluhisho la kidiplomasia zinapofanywa, Marekani huchagua njia ya operesheni za kijeshi zinazoleta hatari kubwa zaidi.

Moja kwa moja

Na Yusuph Mazimu & Mariam Mjahid

Marekani na Iran zarushiana makombora, Trump asema usitishaji wa vita unaendelea

Mvutano kati ya Marekani na Iran umeongezeka tena baada ya pande hizo mbili kurushiana mashambulizi saa 24 zilizopita, katika tukio linalotajwa kuwa jaribio kubwa zaidi kwa sitisho la vita lililodumu kwa mwezi mmoja.

Hata hivyo, Rais wa Marekani Donald Trump amesema makubaliano ya kusitisha mapigano bado yanaendelea.

Iran ilidai kuwa Marekani ilishambulia meli mbili karibu na Mlango wa Hormuz pamoja na maeneo ya raia katika kisiwa cha Qeshm na pwani ya kusini mwa Iran. Jeshi la Iran limesema lilijibu kwa kushambulia meli za kijeshi za Marekani karibu na bandari ya Chabahar.

Kwa upande wake, Jeshi la Marekani (CENTCOM) limesema lilifanya mashambulizi ya kujibu baada ya Iran kutumia makombora, droni na boti ndogo kushambulia manowari tatu za Marekani. Marekani imesema hakuna meli zake zilizoharibiwa na kwamba haitaki kuongeza mzozo huo.

Akizungumza mjini Washington, Trump alipunguza uzito wa tukio hilo akisema, “Walitujaribu leo, nasi tukawajibu vikali,” huku akisisitiza kuwa sitisho la vita bado lipo. Marekani pia ilikuwa ikisubiri majibu ya Iran kuhusu pendekezo la kusitisha mapigano bila kutatua moja kwa moja suala la mpango wa nyuklia wa Iran.

Baada ya saa kadhaa za mashambulizi, televisheni ya taifa ya Iran iliripoti kuwa hali imerejea kawaida katika visiwa na miji ya pwani karibu na Mlango wa Hormuz, huku Iran ikionya kuwa itajibu kwa nguvu mashambulizi yoyote yajayo.