Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Safari ya Rigathi Gachagua kama Naibu wa Rais wa Kenya yafika tamati

Gachagua alitakiwa kujitetea mbele ya Bunge la Seneti mchana huu lakini wakati wake wa kujitokeza bungeni ulipofika, hakuwepo.

Muhtasari

  • Naibu wa Rais Rigathi Gachagua hospitalini huku Seneti ikiendelea kujadili hoja ya kumuondoa madarakani
  • Kesi ya kumuondoa Gachagua madarakani kuamuliwa Jumamosi
  • Sinwar ndiye mlengwa mkuu wa Israel huko Gaza
  • 'Tathmini zaidi' zinaonesha Sinwar amefariki dunia, duru zaiambia BBC
  • Naibu Rais Gachagua ana 'maumivu makali ya kifua'- asema wakili Muite
  • Israel 'inaangalia uwezekano' kwamba ilimuua kiongozi wa Hamas Yahya Sinwar huko Gaza
  • Liam Payne: Tunachojua kuhusu kifo cha nyota huyo wa muziki
  • Naibu Jaji: Majaji watafuata utaratibu wa katiba kesi ya Gachagua ikirejea mahakamani
  • Naibu Rais Rigathi Gachagua ni mgonjwa na yuko hospitalini - Wakili Paul Muite
  • Bangladesh yatoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa zamani Hasina
  • Katiba ya Korea Kaskazini sasa yaitaja Korea Kusini kuwa 'nchi hasimu'
  • Marekani inaifuatilia Israel kuhakikisha haiendeshi 'sera ya kuwaangamiza watu kwa njaa' huko Gaza
  • HRW: Tanzania izingatie haki za binadamu kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa
  • Wanne mbaroni Tanzania kwa kumuua mume wa mdaiwa mkopo
  • Jeshi la Rwanda lakanusha madai ya kuwabaka wanawake katika Jamhuri ya Afrika ya Kati
  • Marekani yashambulia hifadhi za silaha za Wahouthi zilizofichwa chini ya ardhi
  • Rigathi Gachagua:Je, ni kesi gani haswa inayomuandama naibu rais katika seneti?
  • Marekani kutenga dola milioni 425 za msaada wa kijeshi kwa Kyiv, huku Australia ikipeleka vifaru 49 vya Abrams
  • Rigathi Gachagua: Bunge la Seneti Kenya kupiga kura kuhusu hoja ya kumuondoa madarakani Naibu Rais
  • Mbunge aliyewasilisha hoja ya kumuondoa naibu wa rais bungeni Kenya ajipata mashakani
  • Meya na watu wengine 15 waliuawa katika shambulio la Israeli kwenye mkutano wa baraza la Lebanon

Moja kwa moja

Na Asha Juma, Ambia Hirsi & Dinah gahamanyi

  1. Rigathi Gachagua: Bunge la Seneti Kenya kupiga kura kuhusu hoja ya kumuondoa madarakani naibu rais

    Baraza la juu la bunge la Kenya linatazamiwa kupiga kura Alhamisi iwapo litamuondoa Naibu Rais Rigathi Gachagua mamlakani katika sakata ya kisiasa ambayo haijawahi kushuhudiwa nchini Kenya.

    Bunge la Seneti litatoa uamuzi wake mwishoni mwa siku ya pili ya kesi ya kuondolewa madarakani dhidi ya Naibu huyo wa Rais.

    Hii inafuatia kura ya kihistoria iliyopigwa wiki iliyopita katika bunge la kitaifa, kumshtaki Gachagua kwa mashtaka 11 yakiwemo ufisadi, uasi, kuidhoofisha serikali na kutekeleza siasa za migawanyiko ya kikabila.

    Kesi katika Baraza la Seneti ilianza Jumatano baada ya Bw Gachagua mwenye umri wa miaka 59, ambaye pia anajulikana kama "Riggy G", kushindwa katika jitihada nyingi za mahakama kusitisha mchakato huo.

    Anatarajiwa kutoa ushahidi atakapojitetea mbele ya seneti siku ya Alhamisi.

    Unaweza pia kusoma:

  2. Mbunge aliyewasilisha hoja ya kumuondoa naibu wa rais bungeni Kenya ajipata mashakani

    Mbunge wa Kibwezi Magharibi Mwengi Mutuse alijipata katika hali ngumu siku ya Jumatano wakati alipokuwa akihojiwa ndani ya Seneti katika kesi ya kuondolewa madarakani aliyowasilisha kwa bunge dhidi ya Naibu Rais Rigathi Gachagua.

    Naibu Rais Rigathi Gachagua kupitia mawakili wake wazoefu wanaoongozwa na Wakili Paul Muite wanapambana kuhakikisha haondolewi mamlakani baada ya Bunge la taifa mnamo Oktoba 8 kupiga kura kuidhinisha kutimuliwa kwake.

    Mutuse alipata kibarua kigumu kujibu maswali makali ya wakili wa Gachagua Elisha Ongoya ambaye aliupinga ushahidi wake mkuu dhidi ya Bw Gachagua.

    Miongoni mwa tuhuma ambazo wanasheria wa Gachagua walitaka kuzifuta ni pamoja na kuihujumu serikali kwa kupinga hadharani sera zake za kuwahamisha wafanyabiashara kutoka soko la wakulima na kuwapeleka katika eneo jipya katika Barabara ya Outering na ubomoaji wa majengo katika maeneo ya mabondeni.

    Timu ya Gachagua ilitumia kanda za video kuwadhihirishia maseneta kuwa alitoa matamshi akiiomba serikali kuwatendea raia utu na zile zilizoonyesha kuwa baadhi ya kauli zilizotajwa kuchochea ukabila zimekuwa zikitumiwa tangu awali pia na Rais william Ruto na kwamba zilikuwa msingi wa ugavi wa madaraka katika serikali ya sasa ya Kenya Kwanza .

    Mawakili wa Gachagua walitoa video ambapo alitoa matamshi akiiomba serikali kuwatendea raia utu kwa kuzingatia ahadi zake za kabla ya kampeni.

    “Naibu Rais anasema ‘Tusiwe na vita na Wananchi.’. Je, unaona jambo lolote la kuudhi katika taarifa hiyo?” Ongoya alimuuliza, Mutuse aliyejibu , hapana.

    "Anatoa wito wa huruma kwa wananchi. Je, unaona jambo lolote la kukera katika sehemu hiyo?” wakili aliuliza.

    Wakati mmoja kesi hiyo ilipokuwa ikiendelea wakili wa Gachagua, alicheza kanda ya video ambapo Rais Ruto alionekana kwenye mkutano akiwaambia wananchi wa eneo la Mlima Kenya kuwa wana 'share' (hisa) katika serikali- kauli ambayo bunge linasema imekuwa ikitumiwa na Gachagua na inachochea ukabila. Gachagua alisema alijifunza kutumia kauli hiyo kutoka kwa Rais Ruto.

    Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea kusikilizwa na seneti leo asubuhi.

    Unaweza pia kusoma:

  3. Meya na wengine 15 wauawa katika shambulio la Israeli kwenye mkutano wa baraza la Lebanon

    Mratibu maalum wa shughuli za Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Lebanon ameikosoa Israel baada ya mashambulizi ya anga kwenye majengo ya manispaa katika mji wa kusini wa Nabatieh kumuua meya na watu wengine 15.

    Jeanine Hennis-Plasschaert aameyaita mauaji ya meya Ahmad Kahil "ya kutisha" na kusema ukiukaji wowote wa sheria za kimataifa za kibinadamu "haukubaliki kabisa".

    Takriban watu watano kati ya waliouawa katika shambulio la Jumatano walikuwa wafanyakazi wa manispaa walioratibu misaada kwa ajili ya raia waliosalia katika eneo hilo, Gavana wa Nabatiyeh Howaida Turk ameiambia BBC.

    Kaimu Waziri mkuu wa Lebanon, Najib Mikati amelaani shambulio hilo, akisema "lililenga" mkutano wa baraza.

    Shambulio hilo lilikuwa kubwa zaidi dhidi ya jengo la serikali ya Lebanon tangu kuongezeka kwa mapigano ya hivi karibuni, ambayo yalianza takriban wiki mbili zilizopita, na limezua wasiwasi juu ya usalama wa miundombinu ya serikali ya nchi hiyo.

    Msemaji wa jeshi la Israel amesema vikosi vyake vimefanya mashambulizi yakilenga makumi ya maeneo ya Hezbollah katika eneo hilo na kuharibu handaki linalotumiwa na kundi hilo linaloungwa mkono na Iran.

    "Tunajua kwamba Hezbollah mara nyingi hutumia fursa ya vituo vya kiraia," balozi wa Umoja wa Mataifa wa Israel Danny Danon alisema katika mkutano wa Umoja wa Mataifa Jijini New York Jumatano.

    Unaweza pia kusoma:

  4. Ni Alhamisi tarehe 17.10.2024 hujambo na karibu tena kwa matangazo haya ya mubashara