Maandamano yazuka Ukraine kupinga hatua ya Zelensky ya kumfuta Waziri wa Ulinzi

Chanzo cha picha, Getty Images
Maandamano yamekuwa yakifanyika katika miji kadhaa ya Ukraine kupinga hatua ya kushtukiza ya Rais Volodymyr Zelensky kumfuta kazi Waziri maarufu wa Ulinzi Mykhailo Fedorov.
Umati wa watu - wengi wao wakiwa vijana - walikusanyika mjini Kyiv, wakishikilia mabango yaliyoandikwa "Hands off Fedorov" na "Acha kuhujumu ushindi!" na kusema neno "Aibu! kwa pamoja ".
Rais Zelensky hajatoa tamko lolote kuhusiana na uamuzi huo, ambao umeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wachambuzi na baadhi ya mashirika ya kiraia.
Fedorov, mwenye umri wa miaka 35, aliteuliwa Januari mwaka huu lakini amesifiwa kwa kuipa wizara hiyo nguvu mpya, kuongoza harakati dhidi ya ufisadi na kutumia data kuchambua na kujaribu kuboresha utendakazi kwenye mstari wa mbele.
Wabunge walitarajiwa kupiga kura leo Alhamisi kuimuidhinisha aliyependekezwa kuchukua nafasi ya waziri wa ulinzi Ihor Klymenko, ambaye kwa sasa anaongoza wizara ya mambo ya ndani.
Kama sehemu ya mabadiliko ya Zelensky, bunge liliidhinisha uteuzi wa mkuu wa mafuta na gesi wa serikali Serhiy Koretsky kama waziri mkuu, baada ya Yuliia Svyrydenko kujiuzulu mapema wiki hii.
Kumekuwa na uvumi kwamba kufukuzwa kwa Mykhailo Fedorov kulihusishwa na mvutano kati yake na Kamanda Mkuu Oleksandr Syrskyi.
Katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Alhamisi, Fedorov alithibitisha hilo, akisema alikuwa amewasilisha pendekezo kwa Zelensky kuwabadilisha Syrskyi na Mkuu wa Wafanyikazi Mkuu Andrii Hnatov.































