Waandamanaji 10 wamefariki dunia katika vurugu inayoshuhudiwa Tanzania - UN
Umoja wa mataifa kitengo cha haki za kibinadamu umesema kuwa idadi ya waandamanaji waliofariki dunia kufikia sasa tangu maandamano yaanze sambamaba na siku ya uchaguzi nchini Tanzania ni kumi pekee.
''Ripoti tulizopokea zinaashiria kwamba watu takribani 10 wameuawa," yasema Umoja wa Mataifa.
Umoja wa Mataifa pia imetoa wito kwa vikosi vya usalama katika taifa hilo la Afrika Mashariki kutotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji.
"Tumetamaushwa na idadi ya vifo na majeruhi yaliyoshuhudiwa katika maandamano yanayoendelea nchini Tanzania''.Shirika la habari la Reuters lilimnukuu msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kutetea haki za binadamu Seif Magango akisema.
Kauli yao inatolewa wakati fununu zimesambaa kuwa ni takriban watu 700 wamefariki katika maandamano yaliyogeuka kuwa vurugu huko Tanzania bara.
Wakati huo huo, Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International nchini Kenya limeiambia BBC kuwa mawasiliano yamekatizwa katika nchi jirani ya Tanzania na halijaweza kuthibitisha ripoti za vifo.
''Hospitali nchini humo hazikubali kutoa taarifa kwa waandishi wa habari au mashirika ya kutetea haki za binadamu wanapoulizwa kuhusu visababishi.''
Pia unaweza kusoma: