Zuchu atangaza ‘kuvunjika kwa penzi lake na Diamond’

Chanzo cha picha, MITANDAO
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Zuhura Othman maarufu kama Zuchu, ametangaza kuwa yeye na mwenza wake Naseeb Abdul anayejulikana kama Diamond Platnumz wameachana baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa takribani miaka sita.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zuchu ametoa ujumbe mzito akieleza kuwa ameamua kuchukua hatua hiyo bila kinyongo, akisisitiza kuwa sababu za ndani zitabakia kuwa siri yao, huku akibainisha kuwa "riziki imeisha."
Katika ujumbe huo, Zuchu amesema: "Namtakia Nasibu kila la kheri. Nimeamua maamuzi haya bila kinyongo. Kwa sasa focus ni mimi na kazi. ALHAMDULILLAH Nimejaribu nilipopaweza lakini Mungu ana mipango yake."
Ujumbe huo umewaacha mashabiki zake na maswali mengi wakihoji iwapo anamaanisha alichoandika au pengine ilikuwa ‘kiki’.
Ndoa ya Diamond & Zuchu
Diamond Platnumz na Zuchu, walitangaza kufunga ndoa mwanzoni mwa mwezi Juni mwaka jana na wakati huo pia ujumbe wao ulionekana kuchanganya wengi wanaowafuatilia wengine wakidai kwamba wawili hao tayari walikuwa wameachana.
Ndoa yao ilikuwa ya siri na watu walionekana kujitokeza mitandaoni na kuwapa hongera pengine baada ya kuona ujumbe wa mama mzazi wa Diamond, Mama Dangote ambaye kupitia Instagram yake, alithibitisha kuwa wamefunga ndoa.
Aidha, hili linatokea wakati Zuchu anasemeka kuwa mjamzito na anatarajia kupata mtoto na Diamond.
Pia unaweza kusoma:






























