Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Viongozi wa CHADEMA wasimulia adha waliyokutana nayo mikononi mwa polisi Tanzania

Viongozi wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, wameeleza masaibu yaliyowapata walipokamatwa na polisi jijini Mbeya, kusini mwa Tanzania.

Muhtasari

  • Watu laghai wadukua nambari ya WhatsApp ya Gavana nchini Nigeria
  • Wafadhili wa New Zealand wasambaza peremende zenye vichocheo hatari
  • Marekani yaidhinisha mauzo ya silaha ya dola bilioni 20 kwa Israel
  • Ukraine yadungua ndege 17 za Urusi zisizo na rubani
  • Uvamizi wa Ukraine nchini Urusi: Tunachojua kufikia sasa
  • Urusi: Hali katika eneo la Belgorod 'ni tete', - Gavana
  • Marekani: Polisi ashtakiwa kwa kumpiga risasi mwanamke mjamzito
  • Mwanajeshi wa Marekani akiri kosa la kuuza siri za kijeshi kwa China
  • Marekani yasema inalenga 'kupunguza joto' huko Mashariki ya Kati
  • Rukia Bulle wa Kenya ashinda Tuzo ya BBC Komla Dumor 2024
  • Waziri wa Israeli ashutumiwa kwa kufanya maombi ya Wayahudi eneo takatifu la Jerusalem
  • Mapacha waliozaliwa tu wauawa baba yao akiwa ameenda kuwasajili huko Gaza

Moja kwa moja

Asha Juma

  1. Waziri wa Israeli ashutumiwa kwa wito wa maombi ya Wayahudi katika eneo takatifu la Jerusalem

    Waziri wa siasa kali za mrengo wa kulia wa Israel amewaongoza mamia ya Waisraeli wa Kiyahudi kwenye eneo takatifu linalozozaniwa mjini Jerusalem, huku wengi wakienda kinyume na marufuku ya muda mrefu ya serikali ya Israeli ya kuomba sala za Kiyahudi eneo hilo.

    Ziara ya Waziri wa Usalama wa Kitaifa Itamar Ben-Gvir katika eneo la Msikiti wa al-Aqsa, unaojulikana kwa Wayahudi kama Mlima wa Hekalu, kumeshutumiwa kuwa kitendo cha uchochezi na viongozi wa Palestina, Marekani, Ufaransa, Umoja wa Mataifa na mataifa kadhaa ya Kiarabu.

    Bw Ben-Gvir alisema kwenye video kwamba "sera yetu ni kuwezesha maombi ya Wayahudi".

    Lakini afisi ya waziri mkuu wa Israeli ilisisitiza kwamba hakuna mabadiliko katika makubaliano ya hali ya sasa ambayo inaruhusu Waislamu pekee kufanya sala zao katika eneo hilo.

    Mahali hapa ni patakatifu zaidi kwa Wayahudi kwa sababu palikuwa na mahekalu mawili yaliyopo kwenye Biblia. Ni sehemu ya tatu takatifu kwa Waislamu, wanaoamini kuwa ni mahali ambapo Mtume Muhammad alipaa hadi mbinguni.

    Ikiwa liko katika Jerusalem Mashariki, eneo hilo lilitwaliwa kimabavu na Israeli kutoka Jordan katika vita vya Mashariki ya Kati vya 1967.

    Chini ya hali ilivyo kwa sasa, Jordan iliruhusiwa kuendelea na jukumu lake la kihistoria kama mlinzi wa eneo hilo, huku Israeli ikichukua udhibiti wa usalama na ufikiaji wake.

    Wapalestina wanaishutumu Israeli kwa kuchukua hatua za kuhujumu mipango hiyo na kulalamika kwamba katika miaka ya hivi karibuni Wayahudi mara nyingi wameonekana wakisali bila kuzuiwa na polisi wa Israeli.

    Video zilizoshirikishwa kwenye mitandao ya kijamii siku ya Jumanne, zilionyesha makundi ya Waisraeli wa Kiyahudi wakiimba wimbo wa taifa wa Israeli, wengine wakiwa wamebeba bendera za Israeli na kadhaa wakiwa wanafanya sala kwenye ukingo mwa eneo takatifu.

    Akitembelea eneo hilo akiwa anasindikizwa na polisi wa Israeli, Itamar Ben Gvir, alisema "hatua kubwa" imepigwa na serikali ya Israeli katika "utawala na uhuru" kwenye eneo hilo. "Sera yetu ni kuwezesha maombi ya Wayahudi," aliongeza.

    Pia alitangaza kwamba Israeli "lazima ishinde vita" katika Ukanda wa Gaza, na haipaswi kuhusika katika mazungumzo ya kusitisha mapigano na kuachiliwa huru kwa mateka ili "kuisambaratisha Hamas".

    Hata hivyo, baadaye, ofisi ya Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu ilisema tukio hilo "limeenda kinyume na hali ilivyo."

    “Sera ya Israeli kuhusu Mlima wa Hekalu haijabadilika; hivi ndivyo imekuwa na hivi ndivyo itakavyokuwa,” ilisisitiza.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Mapacha waliozaliwa tu wauawa baba yao akiwa ameenda kuwasajili huko Gaza

    Mapacha waliozaliwa tu wameuawa katika shambulizi la anga la Israeli huko Gaza wakati baba yao alipokuwa kwenye ofisi ya serikali ya mtaa kuandikisha kuzaliwa kwao.

    Asser, mvulana, na Ayssel, msichana, walikuwa na umri wa siku nne tu baba yao Mohammed Abu al-Qumsan alipokwenda kuchukua vyeti vyao vya kuzaliwa.

    Akiwa bado yuko huko, majirani zake walimpigia simu kumwambia kuwa nyumba yao huko Deir al Balah imerushiwa bomu.

    Shambulizi hilo pia lilimuua mkewe na bibi ya mapacha hao.

    "Sijui ni nini kilitokea," alisema. "Nimeambiwa ni kombora ambalo lilishambulia nyumba." "Sikuwa na wakati hata wa kuwasherehekea," aliongeza.

    Wizara ya afya ya Gaza inayosimamiwa na Hamas inasema watoto 115 wamezaliwa tu na kisha kuuawa wakati wa vita.

    Kulingana na shirika la habari la AP, familia hiyo ilifuata amri ya kuhama mji wa Gaza katika wiki za mwanzo za vita vya Israeli na kutafuta hifadhi katikati mwa ukanda huo, kama jeshi la Israeli lilivyoagiza.

    BBC imelitaka jeshi la Israeli kutoa maoni yake kuhusu shambulizi hilo, na inasubiri majibu.

    Israeli inasema inajaribu kuepuka kuwadhuru raia na inalaumu Hamas kwa vifo vyao, kwa madai kuwa inaendesha shughuli zake katika maeneo yenye makazi ya watu wengi, ikiwa ni pamoja na kutumia majengo ya kiraia kama makazi.

    Lakini ni mara chache sana maofisa hutoa maoni juu ya mashambulizi yanayofanywa moja moja.

    Makaazi kadhaa ya aina hiyo huko Gaza yameshambuliwa katika wiki chache zilizopita.

    Siku ya Jumamosi, shambulizi la anga la Israeli dhidi ya jengo la shule linalohifadhi Wapalestina waliokimbia makazi yao katika mji wa Gaza liliua zaidi ya watu 70, mkurugenzi wa hospitali aliambia BBC.

    Msemaji wa jeshi la Israeli alisema shule hiyo "inatumika kama kituo cha kijeshi cha Hamas na wanajihadi wa Kiislamu", jambo ambalo Hamas ilikanusha.

    Israeli ilipinga idadi ya waliofariki iliyotolewa, lakini BBC haikuweza kuthibitisha takwimu hizo kutoka pande zote mbili.

    Soma zaidi:

  3. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara ya tarehe 14/8/2024