Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Jenin: Waombolezaji wajaza mitaa ya Jenin huku Israeli ikisitisha mashambulio

Mazishi ya watu waliouawa Jenin yamekuwa yakifanyika leo asubuhi

Moja kwa moja

  1. Jenin: Vikosi vya Israel vyaanza kuondoka baada ya operesheni ya siku mbili

    Vikosi vya Israel vimeanza kuondoka katika kambi ya wakimbizi ya Jenin katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, chanzo cha ulinzi kinasema.

    Hii inahitimisha operesheni kubwa ya siku mbili ambapo Wapalestina 12 na mwanajeshi mmoja wa Israel wameuawa.

    Milio ya risasi na milipuko viliweza kusikika katika kambi ya Jenin wakati habari zilipoibuka Jumanne jioni.

    Jeshi la Israel lilisema baadaye kuwa lilinasa makombora matano yaliyorushwa kuelekea kusini mwa Israel na wanamgambo wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza.

    Hakuna kundi lililodai mara moja kwamba lilihusika na mashambulio.

    Wakati Waisraeli wakiendelea kuondoka Jenin, maafisa wa afya wa Palestina waliripoti kwamba mwanamume mmoja wa Kipalestina aliuawa na vikosi vya Israeli. Ilisema alikuwa kifo cha 12 cha Wapalestina katika mji huo tangu Jumatatu.

    Unaweza pia kusoma:

    • Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
    • Mzozo wa Israel na Palestina: Je kuwa na taifa moja ndio suluhisho?
  2. Hujambo na karibu kwa matangazo yetu mubashara leo tarehe 05.07.2023