Michezo ya Olimpiki ya Wamaasai Kenya: Mamia yakusanyika kuwinda mbadala wa simba
Vijana wa Kimaasai nchini Kenya wamekusanyika pamoja kwa ajili ya mashindano ya michezo, yaliyobuniwa kama mbadala wa kuwinda simba - desturi ya kitamaduni ya kuingia utu uzima.
Mamia walichuana katika michezo mbalimbali katika maeneo ya chini ya Mlima Kilimanjaro, ikiwemo kurusha mikuki, riadha na kurukaruka.
Kwa vizazi na vizazi vijana wa Kimasai walitarajiwa kupigana na kuua simba kama sehemu ya utamaduni inayozingatia mabadiliko yao ya utu uzima.
Lakini baada ya idadi ya wanyama hao wakubwa kuanza kupungua barani Afrika, wanamazingira na wazee wa wa jamii hiyo walianzisha shindano lililoitwa Olimpiki ya Wamasai.

Chanzo cha picha, EPA

Chanzo cha picha, EPA

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, EPA

Chanzo cha picha, EPA

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, EPA

Chanzo cha picha, EPA








