Majeruhi wa Liliondo Tanzania walia na usalama wao, baadhi wakidaiwa kukimbilia Kenya kwa matibabu

Maelezo ya video, Majeruhi wa Liliondo Tanzania walia na usalama wao, baadhi wakikibilia Kenya kwa matibabu
Iliyochapishwa

Baadhi ya majeruhi katika makabiliano baina ya jeshi la Polisi nchini Tanzania na jamii ya wamaasai waishio katika eneo la Loliondo Kaskazini mwa Tanzania wamekimbilia nchini Kenya kupatiwa matibabu katika zahanati na hospitali za karibu

Chanzo cha mgogoro huo ni zoezi linaloendelea la uwekaji alama kwenye eneo la kilomita za mraba 1500 kati ya 4000 za eneo hilo la pori tengefu

Serikali imeeleza nia yake ya kuendelea na zoezi hilo kutokana na umuhimu wake kwa ikolojia na uhifadhi wa Wanyama pori nchini Tanzania

Eagan Salla ametuandalia taarifa ifuatayo