Ufahamu mji wa New Zealand ambao unahitaji pasipoti kuingia - je kipi cha mno?

Iliyochapishwa

Kila ifikapo Januari mosi, wageni humiminika katika Jamhuri ya Whangamōmona kusheherekea mahali ambapo ''palikataa kumezwa''.

Wakati mwingine vipengele vya kijiografia vinatajwa ipasavyo, na Barabara kuu ya Ulimwengu Iliyosahaulika ya New Zealand bila shaka ni mojawapo ya hizo.

Kuendesha gari kutoka mji wa Taumarunui hadi Whangamōmona huko Taranaki katika sehemu ya magharibi ya Kisiwa cha Kaskazini cha New Zealand, hukufanya uhisi kama unapitia sehemu ya dunia ambayo imesahaulika wakati huo.

Ni mahali ambapo moas (ndege walio na urefu wa futi 8 waliotoweka sasa) walianguka msituni na mizabibu minene ya kijani kibichi na matawi yaliyojipinda yalizunguka miti ya kale ya kauri na totara, giza lililoangaziwa tu na miale ya ajabu ya mwanga wa kijani kibichi unaopenya kwenye mwavuli wa msitu.

Barabara ya km 87 imepinda na haisameheki, lakini vichaka safi na tandiko za mandhari nzuri huifanya iwe ya thamani, unapoendesha gari kuelekea Jamhuri ya Whangamōmona, kama vile wenyeji hupenda kuiita wakati mwingine.

Mji huu mdogo, wa mbali unajulikana sana nchini New Zealand kama mahali palipokataa kumezwa na kanuni mpya za eneo mwishoni mwa miaka ya 1980 na hivyo kujitangaza kuwa huru.

Una 'pasipoti'yake

Kwa hakika, ukitokea Siku ya Jamhuri, inayoadhimishwa kila baada ya miaka miwili mwezi wa Januari, huwezi kuingia mjini bila pasipoti hiyo.

Gaylene Coplestone anakumbuka vizuri.

''David Walter alikuwa meya wa Halmashauri ya Wilaya ya Stratford [mji mkubwa wa karibu zaidi] wakati huo. Alikuwa rafiki yetu mzuri na ni wazi alihusika sana katika siasa za mitaa. Hakufurahishwa sana walipotangaza mipaka inakwenda kubadilishwa.''