Urusi na Ukraine: Ni zipi athari za kuzama kwa meli ya kivita ya 'Moscow' katika vita vya Urusi na Ukraine?

रशिया-युक्रेन युद्ध

Chanzo cha picha, MAX DELANY/AFP

Iliyochapishwa

Meli ya kivita ya Urusi iliharibiwa na kuzama katika Black Sea. Urusi na Ukraine zinaafiki kuhusu kuzama kwa meli hiyo. Lakini kuna tofauti baina ya nchi hizi mbili kuhusu sababu ya meli hiyo ya kivita kuzama.

Kwa mujibu wa Wizara ya ulinzi ya Urusi, meli ya kijeshi yenyewe iliharibiwa na moto uliotokana na risasi zilizokuwemo ndani ya meli. Meli ilizama Ilipokuwa njiani kuelekea kwenye bandari.

Wakati huo huo huo, Ukraine inadai kuwa iliishambulia meli ya kijeshi kwa kombora aina ya Neptune . Afisa wa Marekani, akiongeza kwa sharti la kutotambuliwa utambulisho wake kwa kuwa hakupewa ruhusa ya kuongea na vyombo vya habari, alisema katika taarifa kwamba Marekani halina mipango ya kushitaki Ukraine.

Ifahamike kuwa wanajeshi wa majini 510 walikuwa katika meli za kivita za Urusi. Ndege ya kivita ilikuwa ikiongoza harakati za kivita dhidi ya Ukraine kwa njia ya bahari. Kwasababu ya hili, kuzama kwake ni muhimu kijeshi na kama alama.

Unaweza pia kusoma:

मॉस्कवा

Chanzo cha picha, MAX DELANY/AFP

Maelezo ya picha, Moscow ilipata umaarufu mwezi Februari, siku ambayo Urusi iliivamia Ukraine.

Ndege ya kijeshi ilitoa wito wa kujisalimisha kwa kikundi kidogo cha wanajeshi wa Ukraine waliohusika katika ulinzi wa kisiwa cha nyoka (Black Sea island of Snake). Lakini walikataa kufanya hivyo .

Risasi au shambulio la kombora?

Kabla ya Kuzama kwa meli ya Moscow, Wizara ya ulinzi ya Urusi ilikuwa imetoa taarifa ikisema "meli ya kivita yenyewe ilikuwa imeharibika na mabaharia wote walikuwa wameokolewa ."

Jumanne (Aprili 14) mchana, Wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema meli hiyo ilipatikana ikiwa inawaka moto na kwamba ilikuwa inapelekwa kwenye bandari.

Taarifa nyingine iliyotolewa baadaye ilisema kuwa meli hiyo ya kivita ilizama kutikana na hali kama ya Dhoruba iliyotokea ndani ya bahari.

मॉस्कवा

Chanzo cha picha, Reuters

Hata hivyo Ukraine inadai kuwajibika kwa kuzama kwa meli hiyo. Inadai meli hiyo ililengwa na makombora ya Neptune yaliyotengenezwa nchini Ukraine.

Kabla ya kuzama, maafisa wa Ukraine walisema kwenye ujumbe wa Facebook kwamba mlipuko katika meli ya kivita ya Urusi na hali mbaya ya hewa vimesababisha ugumu wa kuwaokoa watu waliokuwemo ndani yake.

Maafisa wa Marekani na Ukraine walisema makombora ya Neptune yaliipiga meli hiyo. BBC bado haijathibitisha dai hilo .

Historia ya meli ya Moscow

Meli hiyo ya kijeshi ilitengenezwa wakati wa enzi ya Usovieti. Meli hii ilianza shughuli zake katika miaka ya themanini na imekuwa ikiiwakilisha Urusi katika Bahari nyeusi tangu mwaka 2000.

Tangu Urusi kulitwaa jimbo la Crimea mwaka 2014, Bahari nyeusi imekuwa ikitawaliwa na wanajeshi wa Urusi .

मॉस्कवा

Chanzo cha picha, REUTERS/DENIS SINYAKOV

Hata wakati wa mzozo wa sasa, msafara uliopo katika Bahari nyeusi unaweza kufyatua makombora kokote ndani ya Ukraine . Zaidi ya hayo, vikosi hivi vya wana maji vimekuwa na mchango muhimu katika juhudi za kuiteka Mariopol.

Katika vita vinavyoendelea na Ukraine, Meli hiyo inayofahamika kama Moskva au Moscow ilikuwa imetia nanga karibu na mji wa kusini wa Mykolaiv.Urusi iliripotiwa kuupiga mabomu mji huo hivi karibuni.

Meli hiyo ilidaiwa kuwa na mifumo ya kuzuwia makombora yanayorushwa kutoka manuari pamoja na silaha nyingine na ilikuwa imetengenezwa na kinga ya kuilinda na mashambulio.

Kuna hiyo ya kijeshi huenda ilizama kwa shambulio la Ukraine, lakini itakuwa ndio meli kubwa kuzama tangu kumalizika kwa Vita vya vikuu vya II vya dunia.

Meli hiyo inasemekana kuwa na uzito wa tani 12,490.

Moscow ilikuwa imara

Jonathan Bentham, mtaalamu wa jeshi la majiji katika taasisi ya masomo ya stratejia , aliambia BBC kwamba Moscow ilikuwa meli thabiti. Meli hii ya kivita ilikuwa inachukuliwa kama meli salama zaidi miongoni mwa meli zote za Urusi zinazofanya kazi.

Meli hiyo ilikuwa na vifaa vyote ikiwa na mataili matatu ya mfumo wa ulinzi dhidi ya mashambulio ya anga . Iwapo ungetumiwa vyema, mfumo huu unaweza kutoa fursa tatu za ulinzi dhidi ya mashambulio ya makombora ya Neptune.

EPA

Chanzo cha picha, Getty Images

Kulingana na Bentham, Moscow ingekuwa uwezo wa nyuzi 360 za eneo la kujikinga na mashambulio ya anga.

Mashambulio ya hivi karibuni katika mji mkuu wa Kiev, na Lviv yamelenga ngome kadhaa za kijeshi za Ukraine.

Msemaji wa wizara ya ulinzi Igor Konshenkov alisema makombora, ambayo yana umwezo wa kupiga maeneo yaliyokusudiwa, yalipiga maeneo 16. Maeneo haya ni kuanzia kutoka kombora la Neptune kwenye viwanda vya silaha na kwenye magala ya silaha.

Wakati huo huo, Mwandishi wa BBC Tom Bateman aliyeko Denipro anaripoti kuwa Urusi inaangalia uwezekano wa kuwazuwia watu kabisa kutoka au kuingia katika Mauripol kuanzia Jumatatu.

Unaweza pia kusoma: