Mzozo wa Sudan: Waandamanaji walioapa kupigania uhuru wao Sudan

Waandamaji wameapa kuendelea kushikilia msimamo wao

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa

"Je, nilinusurika kwenye mauaji?" aliuliza kijana wa Sudan alipojibu simu yangu muda si mrefu baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi waandamanaji katika jiji la Khartoum.

Anajulikana kwa jina la Bashy kwenye mtandao wa Twitter, alieleza jinsi mmoja wa watu saba alivyofariki Jumatatu alasiri katika mji mkuu.

"Nilikuwa nikiwarekodi waandamanaji na kutembea wakati risasi ilipopenya kifuani mwake; alikufa mbele yangu. Huyo angeweza kuwa mimi!"

Katika miaka yake ya kati ya ishirini, na kwa kawaida akiwa na tabasamu usoni, Bashy amekuwa akiandamana mitaani kwa muda wa miezi mitatu iliyopita.

Kama watu wengi wa wakati wake, ana hasira kwamba jeshi lilinyakua mamlaka Oktoba mwaka jana, zaidi ya miaka miwili tu katika makubaliano kati ya majenerali na muungano wa kiraia kugawana madaraka.

Maisha yalikuwa yakiboreka na mzozo wa kiuchumi ukipungua huku Waziri Mkuu wa kiraia Abdalla Hamdok akiileta Sudan kutoka kwenye baridi kufuatia vikwazo vilivyowekewa nchi hiyo wakati wa utawala wa muda mrefu wa Omar al-Bashir, anayetuhumiwa kutumia nchi hiyo kufadhili ugaidi.

Mafanikio ya kiuchumi ya kipindi cha mpito cha miaka miwili ya kugawana madaraka yamepotezwa na mapinduzi hayo

Chanzo cha picha, AFP

Washirika wa kijeshi wa rais huyo wa zamani walimuondoa madarakani mnamo Aprili 2019 kufuatia maandamano makubwa, lakini walionesha kusita kwao kugawana madaraka na wale waliokuwa mitaani walipowageuzia bunduki katika mauaji mabaya miezi miwili baadaye.

Kelele iliyofuata iliwalazimu majenerali kukubaliana na kipindi cha mpito - lakini kama wengi walivyoshuku, wanajeshi hawakufurahia kamwe mpango huo, na mapinduzi ya hivi punde, wanasema, yamewathibitishia kuwa sahihi.

'Mzunguko mbaya'

Bashy, ambaye amekuwa mstari wa mbele katika maandamano ya hivi majuzi yanayoandika kumbukumbu za mikutano na maandamano kwenye mitandao yake ya kijamii, anasema wale walio kwenye kamati za vitongoji zinazoratibu mapambano hayo mitaani ni vijana hasa.

Zaidi ya nusu ya idadi ya watu wa Sudan kwa kiasi kikubwa waliyajua maisha chini ya Omar al-Bashir

Chanzo cha picha, AFP

Kwa hakika inakadiriwa kuwa 61% ya wakazi wa Sudan ni chini ya umri wa miaka 25 na wamechoshwa na kile ambacho Bashy anakiita "utawala wa mtu mwenye mabavu".

Ni mzozo wa vizazi na vijana wanaotaka mustakabali wenye usawa, amani na demokrasia. "Sisi ni tofauti na vizazi vilivyopita," anasema Bashy.

"Tunataka kusitisha mzunguko huo, mzunguko huu mbaya wa mapinduzi ya kijeshi na ubabe. Ndiyo maana tunapinga - kwa sababu tunataka kuona mwisho wa mzunguko huu."

Waaminifu wamerejeshwa

Waandamanaji wanahisi kuwa wana uhalali upande wao - na serikali ya kijeshi imepata pigo kwa kujiuzulu mapema mwezi huu kwa Bw Hamdok.

Baada ya mapinduzi hayo aliwekwa chini ya kifungo cha nyumbani - lakini akasaini mkataba mpya na majenerali - jambo ambalo muungano wake wa kiraia, Forces for Freedom and Change (FFC), ulikataliwa. Alidumu kwa wiki sita tu kabla ya kugundua kuwa hangeweza kufanya kazi bila uungwaji mkono wa kisiasa wa FFC. Baadhi ya mageuzi ya kiuchumi aliyoyaleta - yakishangiliwa na jumuiya ya kimataifa - yalikuwa machungu kwa kila mtu.

Hakika, wiki hii, mtawala wa kijeshi wa Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan hatimaye aliteua utawala wa muda, ambao unajumuisha baadhi ya wafuasi hao watiifu kwa Bashir, kuongoza nchi kwenye uchaguzi.

Nidal, ambaye jina lake limebadilishwa ili kulinda utambulisho wake, ni muandamanaji mwenye uzoefu - kwanza akiingia mitaani wakati wa majira ya joto wakati watu walianza kujitolea mitaani.

Jaribio la Jenerali Abdel Fattah al-Burhan kumleta Waziri Mkuu wa kiraia limeambulia patupu

Chanzo cha picha, Getty Images

Anaamini kuwa kitendo kikali cha jeshi kwa waandamanaji - zaidi ya 70 wamekufa hadi sasa - kinawalazimisha wanaoandaa maandamano kuwa wa busara zaidi - au kushikamana zaidi.

"Unaweza kuhisi kuwa jeshi linatufanyia upendeleo - wanapoua tuua sisi zaidi , hutusaidia sisi kuja pamoja, kuunda upya hisia zetu za utaifa na kukuza uzalendo mpya wa kujenga nchi mpya."

Tangu uhuru majeshi yamehodhi hisia zozote za uzalendo. Lakini vitendo vyao - haswa vile vya kitengo cha zamani cha wanamgambo, Vikosi vya Msaada wa haraka vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan "Hemeti" Dagolo - na jukumu lao katika mauaji ya Juni 2019 inamaanisha kuwa heshima kubwa waliyopewa imepotea kwa vijana wa Sudan.

Kwa Nidal, maandamano yamekuwa na athari mbaya kwa familia yake: mmoja wa binamu zake mwenye umri wa miaka 18 aliuawa kwa kupigwa risasi na askari mwezi Desemba.

Nilipozungumza naye jioni moja wiki hii alikuwa ametoka tu kwenda kwenye vizuizi mbalimbali huko Khartoum ili kuwakusanya binamu zake wengine wengi ili kuangalia kama wote wako salama.

Bado hali imewafanya waamue zaidi - kwa sababu wanahisi wanaweza kuleta mabadiliko. "Niko tayari kufa," aliniambia.

Uaminifu umevunjika

Katikati ya Januari, serikali ya kijeshi ilitangaza kuwa inaunda kikosi cha kukabiliana na ugaidi ili kukabiliana na changamoto za usalama zinazoletwa na maandamano hayo - ambayo pia yanaathiri uchumi.

Kuwatazama waandamanaji wenye amani kama magaidi kunaonekana na wengi kama kuchukua karatasi kutoka kwenye kitabu cha utawala wa enzi ya Bashir.

Katika taarifa zao, mamlaka zinabainisha ni polisi wangapi wanajeruhiwa wakiwa kazini wakati wa maandamano ya nchi nzima - bila kujali vifo vya waandamanaji.

Wiki hii, kifo cha brigedia jenerali wa polisi kimelaaniwa na waandamanaji kunyooshewa kidole, lakini wanaharakati wanapinga hili na kusema kuwa kinatumika kama kisingizio cha kutumia nguvu zaidi.

Na vurugu za wiki hii zilikuja baada ya kituo cha Al Jazeera ambacho kilikuwa kikibeba mipasho ya moja kwa moja ya maandamano na mikutano hiyo kupigwa marufuku.

Ukandamizaji wa uhuru wa vyombo vya habari umekuwa usiokoma: waandishi wa habari wamepigwa na kushambuliwa, ofisi za vyombo vya habari kushambuliwa na vyombo vya habari vya kimataifa vimepigwa marufuku.

Zaidi ya watu 70 wamepoteza maisha na maelfu wamejeruhiwa tangu Oktoba

Chanzo cha picha, AFP

Kumekuwa na msururu wa shughuli za kidiplomasia ili kuondoa mkwamo huo, ikiwa ni pamoja na mchakato wa mashauriano ulioanzishwa na Umoja wa Mataifa.

Lakini Wasudani wengi hawana imani na Umoja wa Mataifa, ikizingatiwa kuwa wanaungwa mkono na kushindwa kwa makubaliano ya Novemba yaliyoingiliwa na Bw Hamdok.

Na waandamanaji wanataka tu jeshi litoke katika serikali yoyote kwani wanahisi majenerali si wa kuaminiwa.

"Hakuna mazungumzo, hakuna ushirikiano, hakuna uhalali" ni kilio cha maandamano cha harakati za sasa za demokrasia.

Kutokana na hali hii, Marafiki wa Sudan walikutana wiki hii kujaribu kutafuta suluhu.

Kundi hili linajumuisha Marekani, Uingereza, mataifa ya Ulaya na washirika wa kijeshi Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Hata hivyo, Bashy na Nidal wote wanasikika kutofurahishwa na juhudi kama hizo - na wanakubali kwamba jeshi la kukabiliana na ugaidi halitawashinda.

"Sisi ni wa kiwango cha dunia katika upinzani wa amani, mauaji ya Jumatatu hayatatuzuia," Bashy alisema. "Hatuwaruhusu kuchukua damu, jasho na machozi yetu na kuvitumia kwa faida yao wenyewe."