Mauaji ya Kimbari Rwanda: Jinsi mafunzo ya sanaa yanavyowaponya wajane wa mauaji hayo

Iliyochapishwa

Wajane wa mauaji ya kimbari ya Rwanda wamekuwa wakipokea  mafunzo ya sanaa ya michezo ya kijihami  ikiwemo mchezo wa  yoga kama njia ya kupona kutokana na majeraha waliyo nayo kwa miaka mingi kufuatia kupoteza wapendwa wao katika mauaji hayo.

Chini ya mradi uliopewa jina la ‘’ Martial Arts  for  justice’’ au michezo ya kujihami kwa ajili ya haki , ulioanzishwa na Master Dean  raia wa Canada anayeshikilia mkanda mweusi katika Taekwondo,wakufunzi wenyeji   hutoa mafunzo  ya michezo ya kujihami  ikiwemo Yoga kwa wanawake walio na umri zaidi ya 60   kama tiba ya kuponya vidonda visivyoonekana. Waliomaliza mafunzo hayo wanasema yaliwasaidia sana kimwili na kiakili.