Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kifo cha Rais Magufuli: Kuna mambo mazuri aliyoyafanya Magufuli na mambo ambayo hayafurahishi, Zitto
Iliyochapishwa
Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Tanzania ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe asema, huu sio wakati wa kukumbuka ni yapi aliyoyafanya Hayati Rais Magufuli na muda wa kujadili tutamkubukaje utafika. Katika mazungumzo na mwandishi wa BBC Zuhura Yunus jijini Dar es salaam Bw Zitto ameanza kwa kutoa salamu zake za rambirambi kufuatia kifo cha Rais Dkt John Pombe Magufuli.