Maalim Seif Sharif Hamad:Mapokezi ya mwili wa Maalim Seif Zanzibar

- Author, Eagan Salla
- Nafasi, BBC Swahili
- Iliyochapishwa
Mamia ya wazanzibari wanaendelea kumiminika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja vilivyopo mjini Ujunga ambapo ndipo mwili wa aliyekuwa makamo wa kwanza wa Urais Zanzibar utakapoletwa kwa ajili ya dua kabla ya kusafirishwa kijijini kwake Mtambwe, kisiwani Pemba.


















