Polisi wenye silaha za moto watanda katika jiji la Dar es Salaam, Tanzania

Chanzo cha picha, Getty Images
Kumekuwa na ongezeko la Polisi wanaoshika doria katika jiji la kibiashara la Dr es Salaam, Tanzania katika sku ya hivi karibuni.
BBC imeshuhudia Polisi wenye silaha za moto katika makutano ya barabara na vituo vya mabasi ya mwendo kasi, wakiwa na magari ya polisi na magari ya washawasha.
Gazeti la The Citizen, limeripoti kushuhIdua polisi katika maeneo ya Magomeni, Buguruni, Tazara, Ubungo, Uhasibu, Fire na Mwenge.
Kuongezeka ulinzi huo kunakuja huku kukiwa na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu maandamano yanayopangwa kufanyika Julai 7.
Haya yanajiri, siku chache tangu serikali ya Tanzania kusimamisha mikutano ya hadhara ya vyama vyote vya siasa, kwa madai ya kuwepo kwa uwezekano wa uvunjifu wa amani katika kipindi cha Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro ameviambia vyombo vya habari kwamba kuwepo kwa askari hao ni sehemu ya operesheni za kawaida za polisi zinazolenga kulinda raia na mali zao.
Soma Zaidi Hapa:





