Virusi vya corona: Rwanda, Burundi, UAE nazo zawekewa marufuku kuingia Uingereza

Wasafiri wakiwa eneo la kuwasili abiria uwanja wa ndege wa Heathrow

Chanzo cha picha, Reuters

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Rwanda,Burundi na Umoja wa falme za kiarabu zimeongezwa kwenye orodha ya nchi zilizowekewa marufuku ya kuingia nchini Uingereza.

Rwanda na Burundi zinajiunga na Tanzania, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Afrika Kusini ambazo pia zimewekewa marufuku hiyo na Uingereza.

Hatua hiyo inalenga kudhibiti kuenea kwa aina mpya ya kirusi cha Afrika Kusini, na marufuku hiyo inaanza kufanya kazi siku ya Ijumaa saa saba kwa saa za Uingereza

Raia wa Uingereza, Ireland na raia wenye haki ya makazi nchini Uingereza wataruhusiwa kuingia lakini kwa sharti la kujitenga kwa siku 10 wakiwa nyumbani.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Watu wenye ushawishi kwenye mitandao ya kijamii walitembelea Dubai majuma ya hivi karibun ,pamoja na kuwepo marufuku ya kusafiri iwapo hakuna ulazima wa kusafiri.

Walisisitiza kuwa safari zao ni kwa ajili ya kazi, lakini idara ya usafiri imesem misamaha yoyote ya kusafiri ambayo kawaida ipo haitakuwepo, ikiwemo kusafiri kwa sababu za kibiashara.

Pia safari za moja kwa moja za ndege za abiria kutoka Uingereza kwenda Umoja wa falme za kiarabu zitapigwa marufuku.

Dubai

Chanzo cha picha, Getty Images

Kwa nyongeza ya nchi hizo inamaanisha kuwa nchi 33 zimewekewa marufuku hiyo mpaka sasa.

Waziri wa usafiri Grant Shapps amesema abiria wanaoruhusiwa kuingia Uingereza watahitaji uthibitisho kuwa hawana maambukizi ya virusi vya corona kabla ya kuwasili, vinginevyo watapigwa faini ya pauni 500.

Uwanja wa ndege wa Dubai umesema kuwa ndege za moja kwa moja zinazotarajiwa kuwasili Uingereza baada ya saa saba, saa za Uingereza zimeahirishwa na umewaambia abiria waliokuwa wakitarajia kusafiri wasiende uwanja wa ndege.

Shirika la ndege la Etihad pia limesema ndege zake zq abiria wake wanaokwenda Uingereza zitaahirishwa mpaka maelekezo mengine yatakapotolewa na wanafanya mipango na wateja wao kuhusu mipango ya kusafiri.