Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mamlaka ya mkoani Shinyanga yasema hakuna aliyeathirika na ulaji wa nguruwe
Iliyochapishwa
Tayari Serikali ya Wilaya ya kahama imepiga marufuku biashara na ulaji wa nguruwe katika eneo hilo ikilenga kutafuta kiini cha ugonjwa huo ambao umeua zaidi ya nguruwe 500 mpaka sasa.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Anamringi Macha amesema, mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitika kuathirika, lakini madhara ya homa hiyo, imefanya serikali ya wilaya yake, kuchukua hatua za haraka.
Amezungumza na mwandishi wetu Yusuph Mazimu na ameanza kwa kumueleza hatua iliyochukuliwa ni ya kisheria.