Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mgogoro Chadema: Halima Mdee asema hajanunuliwa
Iliyochapishwa
Wabunge 19 wa viti maalum waliovuliwa uanachama wa chama cha upinzani Chadema, wamesema wataendelea kuwa 'wanachama wa hiari' wa chama hicho huku wakipanga kukata rufaa juu ya adhabu walopewa.
Viongozi hao 19 hii leo wakiongozwa na Bi Halima Mdee wamesema kuwa baada ya kuvuliwa uanachama na Kamati Kuu, sasa wataenda ngazi ya juu kimaamuzi, Halmashauri Kuu, ili kukata rufaa.