Mgogoro Chadema: Halima Mdee asema hajanunuliwa

Maelezo ya video, Mgogoro Chadema: Halima Mdee asema hajanunuliwa
Iliyochapishwa

Wabunge 19 wa viti maalum waliovuliwa uanachama wa chama cha upinzani Chadema, wamesema wataendelea kuwa 'wanachama wa hiari' wa chama hicho huku wakipanga kukata rufaa juu ya adhabu walopewa.

Viongozi hao 19 hii leo wakiongozwa na Bi Halima Mdee wamesema kuwa baada ya kuvuliwa uanachama na Kamati Kuu, sasa wataenda ngazi ya juu kimaamuzi, Halmashauri Kuu, ili kukata rufaa.