Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Familia ya Mberesero imesema haijapokea taarifa rasmi kuhusu kifo cha kijana wao
Familia ya mtanzania anayedaiwa kujinyonga gerezani nchini, imesema mpaka sasa haijapata taarifa rasmi ya kifo cha kijana wao huyo, aliyekuwa anatumikia kifungo cha maisha jela, baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika katika shambulio la kigaidi la mwaka 2015 nchini Kenya.
Shambulio hilo lililofanywa katika chuo kikuu cha garisa lilisababisha vifo vya watu 148.
Vyombo vya habari nchini Kenya vimeripoti kwamba, Rashid Charles Mberesero, aliyekamatwa mwaka jana na wenzake wawili, alijinyonga kwa kutumia blanketi, kwenye gereza lenye ulinzi mkali la Kamiti.
Baba wa kijana huyo amezungumza na Scolar Kisanga.