Benjamin William Mkapa: Matukio mbalimbali katika picha

Rais mstaafu wa Tazania, Benjamin Mkapa, aliyeaga dunia siku ya Alhamisi, aliliongoza taifa kwa miaka 10 baada ya uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995

Chanzo cha picha, IKULU TANZANIA

Maelezo ya picha, Rais Mkapa akiaga baada ya kumaliza miaka 10 madarakani
Iliyochapishwa

Benjamin Mkapa aliliongoza taifa la Tanzania kwa miaka 10 baada ya uchaguzi wa kwanza wa kuhusisha vyama vingi mwaka 1995.

Alipokea madaraka kutoka kwa Rais wa pili, Ali Hassan Mwinyi ambaye alibadili sera ya uchumi ya nchi kutoka kwenye ujamaa.

Lakini pia alikuwa Mkapa aliyefanya mabadiliko muhimu yaliyofanya nchi kungia kwenye mapinduzi ya kiuchumi.

Kutoka kushoto Rais wa Awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, Rais wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa awamu ya tano Dkt John Pombe Magufuli

Chanzo cha picha, IKULU TANZANIA

Maelezo ya picha, Kutoka kushoto Rais wa Awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, Rais wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa awamu ya tano Dkt John Pombe Magufuli

Hata baada ya kuondoka madarakani, Bwana Mkapa alifahamika katika kuongoza jitihada kadhaa za upatanishi katika ukanda wa Afrika, ikiwemo kusimamia kupatikana kwa amani nchini Kenya wakati wa vurugu za baada ya uchaguzi mwaka 2008.

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga (wa tatu kutoka kulia) akiwa anapeana mkono na Rais Mwai Kibaki (wa tatu kutoka kushoto) huku aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan (wa pili kutoka kushoto) na hayati Benjamin Mkapa (wa pili kutoka kulia) akiwa pembeni yao wakati wa mkutano na waandishi wa habari nje ya ofisi ya Rais tarehe 24 mwezi Januari 2008 jijini Nairobi, Kenya. Mkutano huu ulikuwa wa kwanza kati ya mahasimu wawili wa kisiasa tangu kuanza mzozo baada ya uchaguzi uliosababisha mauaji ya watu nchini humo.

Chanzo cha picha, Getty Images

Pia aliongoza mazungumzo ya upatanishi nchini Baurundi kati ya Serikali ya nchi hiyo na upinzani mwaka 2016 yaliyokuwa na nia ya kumaliza mzozo wa kisiasa wa muda mrefu.

Bujumbura,Burundi : Hayati Benjamin William (kushoto) Mkapa akiwa na hayati Pierre Nkurunziza (kulia) wakionekana katika mazungumzo tarehe 9 mwezi Desemba mwaka 2016

Chanzo cha picha, Getty Images

Baada ya kustaafu, Benjamin Mkapa kwa namna moja au nyingine alikua mpatanishi wa mazungumzo ya amani ya DRC, Zimbabwe, Sudani Kusini na Burundi. Hayati Mkapa alifanya jitihada za kuhakikisha kuwa Afrika inakuwa sehemu nzuri ya kuishi.

Rais Mkapa alisomeshwa elimu yake ya msingi na sekondari na mamishionari wa Kikatoliki, na kwa maisha yote amekuwa muumini wa madhehebu hayo.

VATICAN CITY- Oktoba 1: Papa Benedict wa 16 alikutana na aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati Benjamin William Mkapa, katika maktaba yake binafsi mwaka 2005

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Aliyekuwa kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Benedict wa 16 alikutana na aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati Benjamin William Mkapa, katika maktaba yake binafsi mwaka 2005