Genge la wahuni linaloogopwa Nigeria

Roland alikuwa mwanafunzi wa kwanza kujiunga Buccaneers, jumuiya ya siri ya wanafunzi nchini Nigeria.
Jumuiya hiyo huwa inafanya ibada za kikatili nyakati za usiku katika maeneo ya porini.
Wanachama wa zamani, wanaimba , wanacheza na kunywa huku wakiwa wametengeneza mzunguko na wengine wakiwa wamezungushwa kitambaa kufunika macho wanawapiga sana mpaka majira ya alfajiri.
Ibada hiyo ilikuwa inalenga kuondoa hofu kwa wale ambao walikuwa dhaifu na kuwapa ujasiri.
"Wakati ambao unajumuika katika jumuiya hiyo huwezi kutoka , unakuwa mtu tofauti," Roland aliiambia BBC.
Jumuiya hii, pia , ilijulikana chuo kizima kwa majina la Waharamia, Mapanga meusi na Eiye (kwa lugha ya Yoruba ina maanisha ndege).

Kuna mnyororo wa mamlaka kama ilivyo kwenye kikosi cha jeshi.
Wanatumia maandishi ya siri na wanachama huwa wanabeba silaha zao maarufu kwa ajili ya ibada yao pamoja na rangi zao.
Wanachama wanahaidi kutoa ulinzi dhidi ya magenge ya kihalifu, lakini kikubwa ni kundi ambalo linahusiana na mamlaka na umaarufu.
'Taarifa za uzushi' kuhusu mashambulio ya magenge ya kihalifu
Ibada hizi huwa zinatoa shutuma za uwepo wa vurugu kubwa zinazojumuisha mauaji katika mazingira ya chuo na mara nyingine kuwanyanyasa walimu wa chuo kwa ajili ya kupata alama nzuri katika masomo.
Mara nyingine wanafunzi hupewa ahadi za fursa za mitandaoni.
Matukio mengi yapo hata nje kidogo ya chuo na wanachama wake hawajawahi kwenda chuo. Wanaongeza uwepo wa uhalifu.
Katika maeneo ya miji ya kibiashara kama Lagos ambako ni kitovu cha biashara ya mafuta, wamekuwa wakikusanya vijana wadogo katika makundi ya kihalifu na kutoa mafunzo kwa makundi hayo kama wakiingia chuo.

Mwezi Aprili, wakazi wa Lagos na jimbo la jirani la Ogun waliamua kuunda kundi la kutoa taarifa kuhusu kusambaa kwa makundi ya kihalifu ambayo yana mamia ya genge la wahuni linalojulikana kama 'One Million Boys na Awawa Boys ambayo yalivamia maeneo ya jirani.

Chanzo cha picha, Other

Wakati wa marufuku ya kutoka nje kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona na baadhi ya wakazi walisema kuwa wahuni hao wamekuwa hatari zaidi na wanavamia nyumba za watu.
Hivi karibuni kumekuwa na ripoti nyingi haswa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu magenge hayo ya wahuni kuvamia watu na katika jumuiya nyingine tatizo limeonekana kuwa kubwa zaidi ni kama mashambulizi yanatokea zaidi.
Polisi wanakanusha kuhusika kusambaa kwa wezi hao katika jimbo hilo na kudai kuwa ni taarifa za uzushi, kusema kuwa kuna taarifa za kusambaa kwa magenge ya wahuni katika jimbo hilo kunasababisha hofu na kunaweza kusabisha mashambulizi hayo kuanza kutokea.
Zaidi ya washukiwa 200 walikamatwa na polisi kwa kuhusika katika vita ya genge la wahuni iliyotokea mara baada kiongozi wa kikosi hicho kufariki katika ghasia hizo.
Kwa nini aliingia katika kundi hilo
Roland aliamua kujiunga katika kundi hilo ili kupata ulinzi akiwa chuo mashariki mwa Nigeria.
Rafiki yake aliibiwa na kundi la wahuni na Roland akahusishwa na tukio hilo katika mazingira mawili.

Aliripoti shambulio hilo katika mamlaka ya chuo lakini walinzi wa chuo hawakumsaidia sana.
Walinzi hao ambao hawana silaha hawakuweza kufanya lolote na hawakuwa sawa na wanachama wa mashoka meusi ambao walikuwa wanabeba bunduki na silaha nyingine kubwa.
Waanzilishi wa asili, maarufu kama ukuu Saba, walikuwa wamejitolea kwa mandhari ya maharamia. Walikuwa wakijifinya wao ni maharamia, walivaa vitambaa na kubeba miiko.
"Tulikuwa tukifurahiya na mwelekeo wa kijamii," Soyinka aliiambia BBC.
Alifafanua uhusiano wa sasa kama "watu wabaya, waovu".
"Sikuwahi kufikiria kwamba kikundi chochote kinachotegemea chuo kikuu kinaweza kuiga au kutumia mfumo wa mafia, ambao ulihusisha vitendo vya vya ubakaji, wizi, mauaji, utekaji nyara.

"Sikufikiria kwamba kitu chochote kinaweza kudhoofika. Na kwa nini ilidhoofika? Badala ya watoto hawa kuhusishwa kama wahalifu, walikuwa wakilindwa na wazazi wao na ndugu zao wakaribu, "alisema.Soyinka bado ni mwanachama, sasa inapatikana kama kikundi kilichowekwa kwa "juhudi za kibinadamu na za huruma".
Haiwaajiri tena wanafunzi, na uongozi wake ukaondoa vyuo vikuu mnamo 1984 ili kuwatenga na vurugu.

Chanzo cha picha, Getty Images
Jinsi jamii zilivyokuwa na vurugu
Mgawanyiko katika maharamia mwishoni mwa miaka ya 1960 ulisababisha wanafunzi waliohitimu kuanzisha Buccaneers, na jamii zingine.
Uhasama ukaanza mdogo mdogo baina yao walipojigamba kwa ufahari, madaraka, wanawake na urahisi wa kuonana wanasiasi mafisadi ambao walianza kuajiri washiriki wa ibada ya kutoa vurugu dhidi ya wapinzani.Vikundi vingine vinavurugu zaidi kuliko vingine na sio washiriki wote wanaohusika katika uhalifu. Walakini, wote walitengeneza woga mioyoni mwa Wanaigeria.

Shoka jeusi ni kati ya kikundi chenye sifa mbaya zaidi. Waliibuka katika miaka ya 1970 na hapo awali walijulikana kama wanaharakati weusi. Waanzilishi wake walisema lengo la kikundi hicho ilikuwa "kukomboa" watu weusi.
Lakini katika vyuo vikuu, kundi hilo halionekani tena kuwa linaendeshwa na itikadi yoyote ya kisiasa.
Badala yake, washiriki wa shoka jeusi wanashutumiwa kwa mauaji mengi na mashambulio ya kingono.
Tuhuma za kijeshi kufadhili ibada hizo za kikatili
Mnamo mwaka wa 1999 waliwauwa washiriki watano wa umoja wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Obafemi Awolowo katika jiji la kale la Ile-Una katika Jimbo la Osun.
Washiriki wa shoka jeusi pia wamekuwa wahasirika wa dhuluma za kikatili.
Katika Chuo Kikuu cha Port Harcourt katikati ya miaka ya 1990, kiongozi wa ibada hiyo aliachishwa kazi na kichwa chake kilichojaa damu kiliwekwa kwenye mti mlangoni mwa chuo kikuu kama ishara ya ushindi.
Vurugu hizi za vyuo vikuu vimepungua katika miaka ya hivi karibuni
Ilikuwa mbaya zaidi katika miaka ya 1980 na 1990 wakati Nigeria ilishuhudia mapinduzi kadhaa.
Jeshi lilishutumiwa mara kwa mara juu ya ufadhili na kununuliwa vitambulisho kushambulia na kukandamiza harakati za maandamano ya wanafunzi kutaka demokrasia.

Mara chache sana wanachama huacha ibada wakati bado wapo vyuo vikuu - wale ambao wanathubutu kufanya hivyo wanapigwa au, kwa hali nyingine, kuuawa.
Wanafunzi wengine wameacha masomo yao ili kuepukana na ujanja wa ibada hizo.

Chanzo cha picha, Getty Images
Wengine hubaki washiriki wa mambo hayo maisha yao yote. Inawapa fursa za mitandao kupata kazi nzuri na kupata nguvu.
Pia hufadhili ibada, ambazo washiriki wao hufanya kama pimps. Wanawaunganisha na wanafunzi wa kike, wakati mwingine kwa mazoezi ya ngono yanayohusu wanasiasa na wafanyabiashara.
Roland anaamini ibada hizo hutoa maoni ya uwongo ya usalama, ufahari na nguvu. Wanachama daima wako kwenye makali, hawajui ni lini kundi la wapinzani litashambulia.
"Nusu ya wakati ungekuwa na hofu. Haijalishi wanasema [wanachama], huwa wanaogopa," alisema.
* Jina la Roland limebadilishwa kwa usalama wake mwenyewe













