Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Je umawahi kuiona ndizi ghali zaidi duniani?
Iliyochapishwa
Msaani mzaliwa wa eneo la Georgia Marekani, David Datuna amekula ndizi iliyotumika katika kazi ya sanaa ya Maurizo Cattelan ambayo iliuzwa kwa kitita cha dola $120,000.
Sanaa hiyo kwa jina 'Comedian' ilikuwa katika maonyesho ya Sanaa ya Basel mjini Miami Marekani, ambayo ndio sehemu yenye maonyesho ya sanaa zenye hadhi ya juu duniani.
Imewekwa ndizi nyengine hivyo basi hakuna hatua itakayochukuliwa dhidi ya Datuna – ambaye alisema kwamba hatua ya kula ndizi hiyo inaharibu ‘maonyesho ya sanaa’.