Corona: Mwanamziki wa R & B Jeremih apata nafuu

Iliyochapishwa

Mwanamziki wa Marekani mdundo wa RnB Jeremih amesema daima atawashukuru wahudumu na madaktari waliookoa maisha yake baada ya kuugua vibaya virusi vya Covid-19. Nyota huyo sasa anapona nyumbani kufuatia kulazwa wiki kadhaa katika hospitali ya Chicago. Awali iliripotiwa kuwa kwenye mashine ya kumsaidia kupuma, lakini sasa anasema "anazidi kuwa na nguvu kila siku".