Kisima kisichoongezeka maji wala kupungua katika kipindi chote cha mwaka Tanzania

Kisima kisichoongezeka maji wala kupungua katika kipindi chote cha mwaka Tanzania
Iliyochapishwa

Kisima cha Karne ya 13 kilichopo wilaya ya Bagamoyo ni moja kati vivutio vikubwa kwenye makumbusho ya kale ya Kaole.

Maji ya kisima hicho ni baridi licha kuwa karibu na ufukwe wa bahari ya hindi lakini maji yake hayaongezeki wala kupungua kwa kipindi chote cha mwaka licha ya vipindi mbalimbali vya majira ya mwaka.

Eneo hilo la Makumbusho ya Kaole pamoja na kisima hicho pia kuna Mbuyu wenye zaidi ya miaka 600 na kaburi la wapendanao.