Victoria: Malkia aliyekwepa kifo mara 7, aliwezaje kuwakwepa wauaji?

Chanzo cha picha, Getty Images
Ilikuwa Juni 27 1850. Ilikuwa siku ambayo Malkia Victoria alifikishwa kwenye mlango wa kifo. Jioni hiyo alitoka na watoto wake watatu kwenda kumtembelea mjomba wake aliyekuwa anaumwa nyumbani kwake huko Piccadilly.
Maelfu ya wakazi wa London walikusanyika nje kumwona. Wakati wengi wao walikuwa na hamu ya kumuona Malkia Victoria, mtu mmoja alikuwa pale kwa nia tofauti.
Wakati msafara wa kifalme ukisonga mbele, mtu huyo anayeitwa Robert Pate, akiwasukuma watu waliokuwa mbele yake, alikimbia kuelekea lilipokuwa gari la wazi ambalo Malkia alikuwa akisafiria.
Rani akiwa kwenye gari aligongwa kichwani na fimbo ya chuma. Watu wote pale waliingiwa na hofu kutokana na tukio hili. Victoria alisimama katikati ya sekeseke hilo huku akirekebisha kofia yake akasem kwa upole kwamba hakujeruhiwa.

Chanzo cha picha, Getty Images
Hii ni mara ya tano kwa Malkia huyu kushambuliwa tangu awe Malkia mnamo mwaka 1837.
Wakati huo vyombo vya habari vilizungumza mara nyingi juu ya mawazo yake ya utulivu.
Kama ilivyoripotiwa na The Morning Post, aliwasalimia watu wote waliokuwa wakimngojea akirudi kwenye Jumba la Buckingham baada ya tukio hilo.
Ingawa kuna simulizi kwenye vyombo vya habari kuhusu ujasiri wake, uvumilivu na roho ya utulivu, majarida yake ya binafsi yanaonyesha hisia za Victoria.
Aliandika kwamba shambulio dhidi yake lilikuwa kama ndoto mbaya kutoka kwa mtazamo wa usalama wa Jumba la Buckingham.
Aliandika kwamba woga na kuchanganyikiwa kulikosababishwa na tukio hilo kulisababisha hasira... jambo ambalo alihisi ni la aibu na la uoga zaidi.
Sio Victoria pekee bali pia Prince Albert alishtuka katika kuhusu tukio hilo.

Chanzo cha picha, Getty Images
Tukio la kushambuliwa kwa Rani liliamsha hisia miongoni mwetu. "Ni vizuri kupata ajali mara moja moja ili kujua jinsi tunavyopendwa," alitania Victoria.
Aliazimia hatojificha kukwepa tishio la kushambuliwa tena.
Mnamo 1842, Malkia Victoria alikuwa njiani kuelekea Constitution Hill wakati kijana mmoja aitwaye John Francis alielekeza bastola kwenye gari lake.
Lakini, Francis alifanikiwa kutoroka bila kufyatua risasi.

Chanzo cha picha, Getty Images
Waziri Mkuu Robert Peel alimuomba Malkia huyo abaki nyumbani, asitoke. Lakini, malkia alikataa ombi hili. Kwa upande mwingine, timu mpya ya polisi iliyoteuliwa ili kumlinda na kusaidia kumnasa mhalifu anayetaka kumuua.
Jioni iliyofuata, Malkia alitoka akiwa na Albert Rod kwenye gari la wazi. Gari lake lilikuwa limezungukwa na walinzi.
Hapo hapo Francis alijaribu kumshambulia tena. Safari hii alifanikiwa kufyatua risasi. Mara moja alizingirwa na polisi. Kwa bahati nzuri, Malkia alinusurika tena katika tukio hilo. Hakupata majeraha yoyote. Lakini, hali ingekuwa tofauti.
Hata baada ya shambulio la Francis, Malkia alianza tena majukumu yake ya kifalme. Hakutaka kukaa ndani. Alihudhuria hafla za umma. Waandishi wa habari walisifu ujasiri na ushujaa aliouonyesha Malkia.

Chanzo cha picha, Getty Images
Alisifiwa kama Malkia mwenye moyo kama simba, na ingawa alikuwa Malkia kwa jinsia, lakini alikuwa mfalme kwa ujasiri.
Ilikuwa muhimu kwa Malkia Victoria kuonyesha hili hadharani.
Lakini, ni vigumu kusahau uzoefu huo wa kutisha.
Katika miaka ya 1840 Victoria alipigwa risasi na wanaume wanne tofauti. Kufikia wakati wa shambulio la Robert Pate mnamo 1850, Janante alikuwa ameanza kuhisi aina fulani ya wasiwasi ndani yake.
"Watu walipokuja karibu na gari langu nilikuwa na mawazo zaidi ya kwamba wangenishambulia," Victoria aliandika katika jarida lake.
Alitoa hisia zake zenye uchungu zaidi wakati watu aliowapenda walipokufa, lakini si wakati wauaji walipomshambulia.

Chanzo cha picha, Getty Images
Siku chache baada ya mashambulizi ya Robert Pate, rafiki yake na rafiki wa Albert, Robert Peel, walianguka na farasi na kufariki.
Siku chache baadaye, mjomba wake pia alifariki. Aliandika katika jarida lake kwamba aliweza kuepuka hofu, misiba na huzuni iliyosababishwa na vifo hivi.
Hata hivyo, alipatwa na huzuni Albert alipokufa mwaka wa 1861. Kifo cha Albert kilimfanya ahuzunike sana. Baada ya hayo, alijiweka mbali na maisha ya umma.
Kisha akaishi miaka 40 nyingine. Lakini, hakuwahi kupona kutokana na huzuni hii. Alitoka mbele ya umma mara kadhaa na yakafanyika majaribio mengine mawili ya kutaka kumuua.
Majarida yake yanafichua kwamba aliishi katika ulemavu, maumivu na kukata tamaa kwa mwaka mmoja kabla ya kifo chake.
Victoria alinusurika majaribio saba ya mauaji wakati wa uhai wake. Alizaa watoto tisa. Hatua yake ya ujasiri, uvumilivu na kujidhibiti yanasimulia nusu tu ya namna alivyo na simulizi ya yeye ni nani.












