Wafahamu vijana wadogo watoto 5 walioleta mabadiliko duniani

G

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Nkosi Johnson alifariki katika mwaka 2001
    • Author, Dinah Gahamanyi
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Iliyochapishwa

Mara nyingi, vijana wadogo walio katika umri wa kubarehe hufikiriwa kama watu ambao huwa hawana upeo wa juu wa kufikiria mambo, na wakati mwingine huonekana kama wavivu.  Lakini kwa vijana hawa ni tofauti.

1: Nkosi Johnson 

Nkosi Johnson 
Maelezo ya picha, Nkosi Johnson 

Nkosi Johnson  alizaliwa  1989 na kufariki dunia 2001.  Nkosi alizaliwa na maambukizi ya  HIV/AIDS - aliyoyarithi kutoka kwa wazazi wake. Katika mwaka  1997, alikataliwa kujiunga na shule ya umma kwasababu ya hali yake ya HIV.

Hata hivyo alikuwa mwanakampeni mkuu wa jinsi waathiriwa wa HIV wanavyopaswa kuchukuliwa sawa na watu wengine na kwa heshima katika kipindi ambacho kulikuwa na ubaguzi mkubwa dhidi ya watu wenye maambukizi hao.  

Pamoja na mama yake mlezi, alianzisha kituo cha wakimbizi cha akina mama na watoto wao wenye HIV.  Alipokea Tuzo ya Amani ya Watoto . Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela alimuelezea- kama  ‘alama ya mapambano kwa ajili ya maisha.’

2: Malala Yousafzai 

G

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Malala Yousafzai 

Malala Yousafzai  alizaliwa mwaka 1997 nchini  Pakistani. Akiwa mshichana wa shule nchini mwake, alipinga vitisho vya kampeni za kundi la Taliban kwa ajili ya kampeni ya elimu kwa wasichana.

Alinusurika kuuawa baada ya kupigwa risasi kichwani na kuwa mtetezi wa haki za binadamu, haki za wanawake, na haki ya elimu.

Amekuwa akisisitizia asili ya amani ya Uislamu na heshima Uislamu ulionayo kwa elimu.

 Kutokana na hilo Malala amekuwa alama ya  mapambano ya elimu kwa wasichana duniani. 

3: Samantha Smith

Getty

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Samantha Smith

Samantha Smith  alikuwa mwanafunzi msichana  Mmarekani kutoka eneo la Maine. Alizaliwa mwaka  1972 na kufariki 1985.  Katika mwaka 1982, salimuandikia barua kiongozi wa Muungano wa Usovieti  , Yuri Andropov, akimuuliza ni kwanini uhusiano baina ya Marekani na Muungano wa Usovieti ulikiwa wa wasi wasi.

 Barua yake ilichapishwa katika  Pravda, na baadaye  Andropov alimjibu. Smith pia alialikwa kutembela Muungano wa Usovieti  na kwenda.  

Ziara yake ilifuatiwa na taarifa nyingi za vyombo vya habari , ambavyo vilimnukuu    Smith akisema kuwa alikuta Warusi wako tu kama sisi.

Katika mwaka 1983, aliitembelea  Japan, akiwa kama balozi mdogo zaidi wa Marekani. Alifariki akiwa na umri wa miaka 13 pekee, katika ajali ya ndege. 

Emma González

G

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Emma González

Mnamo mwezi wa  Februari 2018,  mtu mwenye silaha alivamia katika shule ya sekondari ya  Marjory Stoneman Dauglasiliyopo  Parkland, Florida,  na kuwauwa watu 17.  

Lakini badala ya  kuathiriwa na tukio hilo baya, vijana wengi walionusurika na ufyatuaji huo wa risasi walianza kampeni ya kitaifa kujaribu kumaliza ghasia za bunduki.

Emma González, wakati huo akiwa na umri wa miaka18 pekee, alijitokeza kama mmoja wa viongozi wa vuguvugu hili jipya na akawa muasisi mwenza wa kikundi kilichozungumzia kuhusu haja ya udhibiti wa silaha kinachojulikana kama Vever Again MSD .

 Mwezi Machi 2018, alitoa hotuba nzito katika maandamano yaliyolenga kuhimiza udhibiti wa silaha nchini Marekani  - March for Our Lives  mjini Washington, D.C. wakati ambapo alisoma wazi majina ya wanafunzi wenzake waliofariki na kukaa kimya kwa mud awa dakika nne- muda uliotumiwa na mshambuliaji kufanya shambulio. 

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

Mwisho wa X ujumbe

Jack Andraka

Getty

Akiwa na umri wa miaka 15 pekee, mwanafunzi wa shule ya sekondari nchini Marekani Jack Andraka alivumbua kile kinachoonekana kama , njia mpya ya kugundua saratani ya kongosho.

Mvulana huyu, ambaye alishinda  $75,000 (£58,000) katika maonyesho ya  kisayansi ya mwaka 2012- Intel International Science and Engineering Fair- kwa ubunifu wake , alisema kuwa alipata wazo hilo kwa kusoma magazeti ya Kisayansi aliyoyapata kwenye mtandao.

Kifaa cha ubunifu wake, ambacho bado kinafanyiwa uchunguzi wa kina, kimetengenezwa kwa karatasi ya kichujio iliyofunikwa na  kimiminika cha chupa zenye kaboni na protini inayoulinda mwili dhidi ya maambukizi (antibody), kulingana na  Wired, na kinahitaji matone sita ya damu ili kupima saratani ya kongosho.