Vikosi vya Ukraine vinarudi nyuma huku Urusi ikiendeleza shambulio la Bakhmut- Uingereza

w

Chanzo cha picha, Reuters

Iliyochapishwa

Wanajeshi wa Ukraine wamelazimika kuondoka katika baadhi ya maeneo katika uwanja wa vita wa mji wa Bakhmut wakati Urusi ikiendeleza mashambulizi mapya huko kwa mizinga mikali katika muda wa siku mbili zilizopita, Uingereza ilisema katika sasisho la kijasusi siku ya Ijumaa.

"Urusi imetia nguvu tena mashambulizi yake katika mji wa Donetsk Oblast wa Bakhmut kwani vikosi vya MoD wa Urusi na Kundi la Wagner vimeboresha ushirikiano," ilisema, ikirejelea wizara ya ulinzi ya Urusi na jeshi lake kuu la mamluki.

"Vikosi vya Ukraine vinakabiliwa na masuala muhimu ya ugavi lakini wamejiondoa kwa utaratibu kutoka kwa nyadhifa walizolazimishwa kukubali," jeshi la Uingereza lilisema katika sasisho la kila siku la kijasusi.

Wagner imechukua uongozi kwa upande wa Urusi katika vita vilivyodumu kwa muda wa miezi kadhaa, vita vya kuua zaidi vya wanajeshi wa pande zote mbili, lakini kiongozi wa kundi la mamluki alilalamikia uungwaji mkono duni kwa vikosi vyake kutoka kwa jeshi la kawaida.

"Ulinzi wa Kiukreni bado unashikilia wilaya za magharibi mwa mji lakini umekabiliwa na moto mkali wa mizinga ya Urusi katika masaa 48 yaliyopita," sasisho la Uingereza lilisema.

w

Chanzo cha picha, Reuters

Ilisema vitengo vya Wagner sasa vinalenga kusonga mbele katikati mwa Bakhmut, wakati askari wa miamvuli wa Urusi walikuwa wakiwatuliza katika mashambulizi kwenye kingo za mji.

Bakhmut, ambayo ilishikilia takriban watu 70,000 kabla ya vita, imekuwa shabaha kuu ya Urusi katika mashambulizi makubwa ya majira ya baridi ambayo hadi sasa yamepata mafanikio madogo licha ya mapigano ya ardhini yakiwa na nguvu ambayo haijaonekana barani Ulaya tangu Vita vya Pili vya Dunia.

Kuteka jiji hilo kungekuwa ushindi wa kwanza kwa Urusi katika kipindi cha miezi minane. Moscow inasema itafungua njia ya kuteka maeneo zaidi katika eneo la Donbas mashariki mwa Ukraine, lengo kuu la vita.

Ukraine, ambayo inajiandaa kwa mashambulizi yake yenyewe, ilionekana kuwa na uwezekano wa kuachana na Bakhmut mwishoni mwa Februari, lakini ilitangaza mwezi Machi kuwa itapigana huko, ikisema Urusi ilikuwa ikipata hasara kubwa zaidi kujaribu kuivamia.