'Nilipoteza mikataba ya kazi baada ya kusema hadharani siko sawa kiakili' - Rosa Ree
'Nilipoteza mikataba ya kazi baada ya kusema hadharani siko sawa kiakili' - Rosa Ree
Iliyochapishwa
Rosa Ree ni mmoja kati ya wanamuziki wakubwa wa Hip Hop nchini Tanzania. Hata hivyo, licha ya ufanisi kimuziki, Rosa Ree alipitia changamoto ya afya ya akili baada ya kujifungua mtoto wake.
Msanii huyo alikumbana na unyanyapaa mkubwa baada ya kujitokeza na kusema kwamba hayuko sawa.
Na hata alipoteza kandarasi na mikataba kadhaa.
Lakini ni nini kilichomsukuma kusema hayuko sawa? Rosa Ree amemsimulia changamoto zake Mtangazaji kinara wa BBC RoncliffeOdit

Chanzo cha picha, Rosa Ree



