Afya: Jinsi ya kufanya kijusi kicheke tumboni?

Chanzo cha picha, Maabara ya utafiti wa vijusi, Chuo kikuu cha Durham
Kulingana na utafiti mpya uliofanywa nchini Uingereza uliowashirikisha wanawake 100 wajawazito na watoto wachanga, watoto katika mfuko wa uzazi "hutabasamu" mama zao wanapoonja mboga za majani(kijani kibichi), na "kugeuza nyuso" wakati wanapokula kabichi.
Ikiwa ladha ya kabichi inakufanya ujisikie,basi hauko peke yako.
Wanasayansi waligundua kuwa kijusi tumboni hutabasamu baada ya kula mboga za kijani kibichi, na kukunja uso baada ya kula kabichi.
Kulingana na Maabara ya Utafiti wa Watoto Wachanga katika Chuo Kikuu cha Durham huko Uingereza, huu ni ushahidi wa kwanza wa moja kwa moja uliorekodiwa unaoonyesha kwamba kijusi hujibu kwa ladha tofauti.
Waliwapa wanawake 35 kidonge chenye unga wa karoti na wanawake wengine 34 kidonge chenye unga wa kabichi. Wanawake 30 waliobaki walijumuishwa katika kikundi cha udhibiti na hawakula chochote.
Kama ilivyoripotiwa na kundi hilo kwenye jarida la "Psychological Science", dakika 20 baada ya akina mama hao kumeza vidonge hivyo, uchunguzi wa 4D ulionyesha kuwa vijusi vya akina mama wengi waliopokea kabichi vilikuwa vimekunja uso, huku wale waliokula mboga za majani hawakutabasamu.
Hakuna matukio kama hayo yaliyojitokeza katika kikundi cha udhibiti kilicho na wanawake wajawazito 30 ambao hawakula chochote.

Chanzo cha picha, Getty Images
Uchunguzi wa awali umeonyesha kwamba mapendekeleo yetu ya vyakula fulani yanaweza kuanzia kabla ya kuzaliwa, kwa sababu maji ya amniotic ambayo yanazunguka kijusi yanaweza kuwa na ladha tofauti kulingana na chakula cha mwanamke mjamzito.
Hata hivyo, kulingana na matokeo ya utafiti huu mpya kutoka Chuo Kikuu cha Durham, utafiti huu ulichunguza kwa mara ya kwanza jinsi watoto wasiozaliwa wanavyoitikia tofauti za ladha tofauti.
Mtoto huanza kuonja chakula kipya lini?
"Tunajua kutokana na tafiti zilizopita kwamba lishe ambayo kijusi hupata kutoka kwa lishe ya mama ni muhimu sana kwa ukuaji wa afya. Lakini hatujui ni lini hasa ladha inaanza," anasema Nadia Reisland, mkurugenzi wa Maabara ya Utafiti wa Mtoto ya Durham, na mwandishi mwenza wa utafiti.
"Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati wanapendelea sukari mapema wiki ya 14 ya ujauzito," aliambia BBC.
"Katika jaribio letu, tulitoa vidonge vya unga kwa vijusi vya wiki 32 na 36, kwa sababu kwa wakati huu sura zao za uso huonekana kuwa ngumu zaidi.
"Tunataka kuendelea na utafiti wetu na kujua ikiwa wanapendelea ladha ya karoti na kabichi baada ya kuzaliwa kwa njia sawa na walivyofanya wakiwa tumboni.
"Tuna matumaini kwamba baada ya kuzaliwa, watajifunza kuhusu mboga za kijani na kuwa na uwezo wa kula mboga za kijani kwa ajili ya chakula cha afya."
Je, jaribio hili linatuambia nini kuhusu maendeleo ya ladha kwa watoto wachanga?

Chanzo cha picha, Getty Images
Kulingana na Reisland, hii inaonyesha kuwa hisia ya ladha inaonekana mapema sana na inategemea urekebishaji wa mazingira ya chakula.
"Baada ya kupokea chakula hiki kutoka kwa mama mjamzito, hata baada ya kuzaliwa, atazoea chakula hiki na kuendelea kukila."
Ladha chungu inayohusishwa na sumu
Utafiti pia unaonyesha sababu nyingine kwa nini kijusi hukataa ladha chungu.
"Tunaihusisha ladha chungu na hatari. Lakini kwa sababu sio ladha zote chungu zinaonyesha sumu, tunahitaji kujifundisha sisi wenyewe na watoto wetu kuondokana na fikra hizi. Baadhi ya vyakula vyenye uchungu ni vyema kwao."
Hata hivyo, aliongeza kuwa, ingawa picha za ultrasound zinaonyesha kwamba watoto wachanga huitikia ladha chungu kwa njia sawa na watu wazima, bado haijulikani kile wanachohisi.
Tabasamu na kukukunja uso vinaonekana kwenye kwenye ultrasound "inaweza pia kuwa harakati za misuli kujibu ladha chungu," anasema Reisland.
Hata hivyo, aliongeza kuwa, viinitete vinajulikana kubadili sura za uso.
Wanasayansi wengine wanafikiria nini?
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Bonyeza hapa kujiunga
Mwisho wa Whatsapp
Dk. Daniel Robinson, Profesa wa Idara ya masuala maisha ya vijusi katika Shule ya Tiba ya Chuo Kikuu cha Northwestern Feinberg, ambaye hakushiriki katika utafiti,
aliiambia NBC kuwa picha za ultrasound hazipaswi kufasiriwa kuwa zinaonyesha kijusi kikiwa na furaha au kuchukizwa.
Dk. Julie Mennella wa Kituo cha Monella cha Kuhisi Kemikali huko Philadelphia pia hakushiriki katika utafiti huo, lakini ni mtaalamu katika uwanja huo.
Gazeti la The Guardian lilimnukuu akisema kuwa utafiti huu unathibitisha matokeo ya awali kwamba watoto wanaweza kuhisi chakula ambacho mama zao wanakula kupitia ladha ya chakula katika kiowevu cha amnioni.
Chapisho hilo pia linamnukuu Katherine Forestell, profesa katika Chuo cha William and Mary huko Virginia, akisema kwamba jinsi kijusi kinavyoitikia chakula cha mama kinahitaji kuchunguzwa katika siku zijazo.
Beyza Ustun, aliyeongoza utafiti huo, anasema: “Tafiti nyingi zimeonyesha kwamba watoto hujifunza ladha na harufu wakiwa tumboni mwa mama.
"Tunafikiri kwamba kukabiliwa na chakula mara kwa mara kunaweza kuhatarisha fetusi kwa chakula hicho baada ya kuzaliwa, ambayo inaweza kuwa muhimu katika kufundisha tabia ya kula afya."
Kwa hivyo, kwa mtazamo wa vitendo, utafiti huu unaweza kuwaongoza wazazi kuunda mazoea ya kula ya watoto wao ambao hawajazaliwa tangu mwanzo.















