Tetesi za soka Ulaya Jumapili tarehe 12.05.2024

Chanzo cha picha, Getty Images
Mabingwa wa Saudi Pro League Al-Hilal wana uhakika wa kumsajili mshambuliaji wa Tottenham na Brazil Richarlison msimu huu, huku Spurs wakiwa tayari kutoa ofa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Mail)
Tottenham wanaweza kumbadilisha Richarlison kwa Eberechi Eze wa Crystal Palace, 25, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Manchester City kwa winga huyo wa England. (Football Insider)
Napoli wanamlenga mlinzi wa Tottenham na Romania, Radu Dragusin, ambaye alihamia England mnamo mwezi Januari, lakini Spurs wanataka pauni milioni 40 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images
Barcelona na Atletico Madrid wanamlenga mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22, huku Manchester United wakiweka dau la pauni milioni 51.7 kwa fowadi huyo. (Marca - in Spanish)
Manchester United itafufua uhamisho wa kiungo wa Barcelona Frenkie de Jong, 26, baada ya kushindwa kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi mwaka 2022. (Mundo Deportivo - in Spanish).
Meneja Msaidizi Steve McClaren anaweza kubaki Manchester United msimu ujao - hata kama bosi Erik ten Hag na wafanyikazi wengine nyuma ya pazia watafutwa kazi. (Mirror)

Chanzo cha picha, Reuters
Arsenal imeweka wachezaji saba wa kikosi cha kwanza kuuzwa, wakiwemo wachezaji watatu wa kimataifa wa Uingereza - kipa Aaron Ramsdale, 25, fowadi Eddie Nketiah, 24, na kiungo Emile Smith Rowe, 23. (Mirror).
Matumaini ya Arsenal kumsajili kiungo wa kati Mhispania Martin Zubimendi yamefifia baada ya mkufunzi wa Real Sociedad Imanol Alguacil kusema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hatauzwa msimu huu wa joto. (Metro)
Kiungo wa kati wa Ujerumani Pascal Gross, 32, anaweza kuondoka Brighton na kujiunga na Eintracht Frankfurt msimu huu wa joto. (Florian Plettenberg)

Chanzo cha picha, PA Media
Everton wana nia ya kumsajili fowadi wa Leicester City na Nigeria Kelechi Iheanacho, 27. (Football Insider)
Bayern Munich wameonyesha nia ya kumteua mkufunzi wa Crystal Palace Oliver Glasner kama mbadala wa Thomas Tuchel, lakini raia huyo wa Austria, 49, anataka kusalia Selhurst Park. (Sky Sports)
Real Madrid itasubiri hadi baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Borussia Dortmund tarehe 1 Juni ili kutangaza kumsajili mshambuliaji wa PSG na Ufaransa Kylian Mbappe, 25 (Athletic - subscription)











