Mzozo Ukraine: Putin aomba radhi kwa matamshi ya Lavrov kwamba Hitler alikuwa Myahudi -Waziri mkuu Israel

Russia's president Vladimir Putin

Chanzo cha picha, EPA

Iliyochapishwa

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameomba msamaha baada ya waziri wake wa mambo ya nje kusema kuwa kiongozi wa Nazi Adolf Hitler alikuwa na "damu ya Kiyahudi", Israel inasema.

Bw Putin aliomba msamaha huo katika mazungumzo ya simu na Waziri Mkuu wa Israel Naftali Bennett, ofisi yake ilisema katika taarifa.

Akaunti ya Urusi ya mazungumzo hayo haikutaka kuomba msamaha.

Sergei Lavrov alitoa maoni ya awali kujaribu kuhalalisha taswira ya Urusi ya Ukraine kama "Nazi" licha ya ukweli kwamba rais wake ni Myahudi.

Bw Lavrov alizungumza na Televisheni ya Italia siku ya Jumapili, siku chache baada ya Israeli kuadhimisha Siku ya Ukumbusho wa Maangamizi ya Wayahudi - moja ya hafla kuu katika kalenda ya Israeli.

Alipoulizwa ni vipi Urusi inaweza kudai kwamba inapigania "kuondoa Naziify" Ukraine wakati Rais Volodymyr Zelensky yeye mwenyewe ni Myahudi, Bw Lavrov alisema: "Ninaweza kuwa na makosa, lakini Hitler pia alikuwa na damu ya Kiyahudi.

Kwa kuwa Zelensky ni Myahudi inamaanisha kuwa ilikusudiwa. Wayahudi wenye hekima wanasema kwamba watu wanaochukia sana Wayahudi kwa kawaida ni Wayahudi."

Maoni hayo yalizua hasira nchini Israel.

Ujerumani ya Nazi iliwaua Wayahudi milioni sita katika mauaji ya Holocaust katika Vita vya Pili vya Dunia.

Israel ilikuwa imetaka kuombwa msamaha, huku Bw Bennett akisema muda mfupi baada ya kuwa "uongo kama huo unakusudiwa kuwalaumu Wayahudi wenyewe kwa uhalifu mbaya zaidi katika historia na hivyo kuwakomboa wakandamizaji wa Wayahudi kutoka kwa wajibu wao".

Katika taarifa ya Alhamisi, ofisi ya Bw Bennett ilisema kwamba imekubali msamaha wa Bw Putin na "imemshukuru kwa kufafanua mtazamo wake kwa Wayahudi na kumbukumbu ya mauaji ya Holocaust".

Urusi ilisema wawili hao walijadili mauaji ya Holocaust, lakini haikusema Bw Putin aliomba msamaha.

Israel imejaribu kupatanisha Urusi na Ukraine, lakini pia imekabiliwa na ukosoaji kwa kutochukua msimamo mkali dhidi ya Rais Putin.

Vyombo vya habari vya Israel wiki hii viliripoti kuwa Israel inafikiria kuongeza msaada wake wa kijeshi na raia kwa Ukraine.

Unaweza pia kusoma

line

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov alisema nini?

m

Chanzo cha picha, EPA

Wizara ya mambo ya nje ya Israel alisema, 'Rais wa Ukraine Zelensky na Hitler wote wana damu ya kiyahudi'

Lavrov alitoa maoni hayo akijaribu kukanusha taswira ya Urusi juu ya Ukraine kama "Nazi" licha ya ukweli kwamba rais wa Ukraine ni Myahudi.

Wizara ya mambo ya nje ya Israel ilimwita balozi wa Urusi kwa "ufafanuzi" na kumtaka aombe radhi.

Ujerumani ya Nazi iliwaua Wayahudi milioni sita katika mauaji ya Holocaust katika Vita vya Pili vya Dunia.

Bw Lavrov alisema hayo katika mahojiano katika kipindi cha televisheni cha Italia Zona Blanca siku ya Jumapili, siku chache baada ya Israel kuadhimisha Siku ya Ukumbusho wa Maangamizi ya Wayahudi, mojawapo ya matukio muhimu zaidi katika kalenda ya Israel.

Alipoulizwa jinsi Urusi inaweza kudai kwamba inapigania "kuondoa Unazi" Ukraine wakati Rais Volodymyr Zelensky yeye mwenyewe ni Myahudi, Bw Lavrov alisema: "Basi vipi ikiwa Zelensky ni Myahudi."

"Ukweli haukanushi vipengele vya Nazi nchini Ukraine. Ninaamini kwamba Hitler pia alikuwa na damu ya Kiyahudi," akiongeza kuwa "baadhi ya watu wabaya zaidi wanaopinga Uyahudi ni Wayahudi."

Waziri wa mambo ya nje wa Israel alijibu kwa hasira kauli ya Bw Lavrov, akimshutumu kwa chuki dhidi ya Wayahudi.