Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Zanzibar haina mgonjwa hata mmoja wa corona lakini yaonya kuhusu wimbi la tatu la maambukizi
Iliyochapishwa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetangaza kuwa kwa sasa visiwa hivyo havina mgonjwa hata mmoja wa Corona.
Kauli hiyo inakuja wakati ambapo Tanzania inajiandaa na tishio la wimbi la tatu la maambukizi ya virusi vya Corona. Zanzibar ikiwa sehemu ya Tanzania ni miongoni mwa maeneo barani Afrika yanayopokea wageni wengi kutoka mataifa mbalimbali duniani hivyo kuwa katika hatari ya kupata maambukizi ya virusi hivyo.
Waziri wa Waziri wa Afya wa Zanzibar Mansor Mazrui amefanya mahojiano na mwandishi wetu Halima Nyanza.