Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ratiba ya mazishi ya Rais Magufuli kutolewa leo
Iliyochapishwa
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli anatarajiwa kuzikwa nyumbani kwao Chatto, mkoani Geita.
Magufuli amefariki jioni ya siku ya Jumatano jijini Dar es salaam kwa matatizo ya moyo.
Msemaji wa serikali ya Tanzania, Dk Hassan Abbas ameviambia vyombo vya habari vya ndani kwamba, utaratibu wa maizishi yake na ratiba ya maziko utatolewa asubuhi hii na Makamu wa Rais wa Tanzania,Bi Samia Suluhu.