Virusi vya corona: Kenya yarejesha usafiri wa ndege

kenya
Iliyochapishwa

Hakutakuwa na haja ya kujitenga kwa lazima kwa wasifiri na watalii wanaowasili nchini Kenya ikiwa hawaoneshi dalili za ugonjwa wa Covid-19, kulingana na tangazo la serikali.

"Abiria wote hawatalazimika kuwekwa kwenye karantini wanapowasili kutoka maeneo waliotoka ikiwa kiwango cha joto la mwili sio zaidi ya nyuzijoto 37.5 na kama hawana kikohozi cha kuendelea, hawana matatizo ya kupumua na wala kuonesha dalili zingine za mafua. Hili ni muhimu kwasababu hatutarajii mtalii kuja katoka maeneo aliotoa kisha awekwe karantini kwa siku 14."

utalii kenya
kenya
Kenya
Kenya
kenya