Kutana na wanariadha wa Afrika wanaotarajiwa kutia fora kwenye Mbio za Ulimwengu 2022

Iliyochapishwa

Katika mkesha wa mashindano ya Mbio za Ulimwengu yatakayoanza nchini Marekani Ijumaa 15, Julai, BBC Michezo Afrika inaangazia wanariadha Ferdinand Omanyala kutoka Kenya, Tobi Amusan kutoka Nigeria na baadhi ya wenda kasi wengine barani Afrika.

Naye mwendesha baiskeli kutoka Afrika Kusini Louis Meinties- mwafrika pekee aliyewahi kumaliza miongoni mwa kumi bora mashindano ya Tour De France mara mbili anatuelezea ndoto zake kuhusu mashindano ya mwaka huu.