Samatta akumbuka ubingwa wa Afrika 2015 na TP Mazembe

Iliyochapishwa

Fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika inapofanyika Jumatatu Mei 30 mjini Casablanca kati ya Al Ahly ya Misri na Wydad ya Morocco, Nahodha wa Tanzania Mbwana Samatta ambaye alishinda ubingwa huo 2015 akiwa na TP Mazembe ya DRC anaelezea BBC Michezo Afrika kwa nini kutwaa taji hilo ni fahari ya kila mchezaji wa Kiafrika.