Coutinho asema kutua Barca ndoto zimetimia

Iliyochapishwa

Kiungo wa kibrazil Philippe Coutinho amesema uhamisho wake kwenda Barcelona ni ndoto iliyokamilika.

Kiungo huyo alieleza hisia zake za kutimiza ndoto yake alipokuwa akipigwa picha katika uwanja wa Nou Camp wakati klabu yake mpya ilipokuwa ikicheza na Levante.

"Mashabiki wa Barcelona tayari nipo hapa, ndoto zimekuwa kweli natumani tunaonana kesho, " alisema Coutinho kupitia video fupi aliyoiweka katika mtandao wa Twita.