Islamic State ladai kuhusika na shambulio la Ukumbi wa Jiji la Crocus Urusi

Siku ya Ijumaa jioni, watu kadhaa waliojificha walifyatua risasi katika ukumbi wa tamasha wa Crocus City Hall huko Krasnogorsk karibu na Moscow, na kuua zaidi ya watu 130, wakiwemo watoto. Jioni hiyo hiyo, kundi la Islamic State, lilidai kuhusika na shambulio hilo.

Moja kwa moja

Abdalla Seif Dzungu

  1. Je Urusi ilipuuza onyo la Marekani kuhusu shambulio la Crocus?

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Baada ya kila shambulio la kigaidi, maswali yasiyoepukika hutokea. Sababu kwa nini haikuzuiwa au kugunduliwa.

    Hata hivyo, mashambulizi ya hivi majuzi huko Moscow yanazua maswali magumu hasa kwa Vladimir Putin huku kukiwa na mvutano wa kimataifa na kutoaminiana, kutokana na ujumbe wa onyo kutoka Washington.

    Mnamo Machi 7, Marekani ilitoa onyo kwa raia wake, kwamba kulikuwa na uwezekano wa vikundi vya "itikadi kali" kushambulia mikusanyiko mikubwa huko Moscow, haswa katika matamasha.

    Aliwashauri raia wa Marekani waliopo Urusi kuepuka au kutoshiriki katika matukio kama hayo katika muda wa saa 48 zijazo.

    Ingawa muda unaweza usilingane vizuri, matukio na eneo la shambulio la jana pamoja na onyo lililotolewa ni sawa katika maeneo mengi.

    Inaonekana wazi kwamba Washington ilijua au kupokea taarifa za kijasusi kuhusu IS, kundi lililodai kuhusika na shambulio la Moscow.

  2. Meli mbili za Urusi zashambuliwa na Ukraine na kuharibiwa Crimea

    .

    Ukraine inasema kuwa imeshambulia meli mbili za kutua kwa ndege za kivita, kituo cha mawasiliano na miundombinu mingine inayotumiwa na meli ya Urusi ya bahari ya shamu kutoka Crimea.

    Tangazo la mkuu wa jeshi la Ukraine lilisema meli za Yamal na Azov zimeharibiwa.

    Gavana wa bandari ya Sevastopol aliyewekwa na Urusi alisema makombora 10 ya Ukraine yamedunguliwa.

    Urusi pia ilitekeleza shambulio la kombora na ndege zisizo na rubani kwenye mji mkuu, Kyiv, na eneo la Lviv mapema Jumapili.

    Wakazi wa Kyiv walijificha katika vituo vya treni wakati shambulio lilipoanza saa 05:00 (03:00 GMT).

    Wanajeshi wanasema kwamba ulinzi wao ulikuwa umedungua makombora 18 ya Urusi na ndege zisizo na rubani 25 huku kukiwa na uharibifu mdogo tu.

    Takriban makombora 20 ya Urusi na ndege zisizo na rubani saba zililenga "miundombinu muhimu" katika eneo la magharibi la Lviv. Hakuna uharibifu umeripotiwa.

  3. Uchaguzi wa urais Senegal: Macky Sall na Ousmane Sonko wazungumza

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Macky Sall

    Baada ya kutekeleza haki yake ya kiraia katika kituo cha Thierno Mamadou Sall huko Fatick (katikati) akiambatana na mke wa rais Marième Faye Sall, Rais anayemaliza muda wake Macky Sall alizungumza na waandishi wa habari, akiwataka wagombeaji wajizuie.

    “Sio juu ya mgombea wala kambi kutangaza ushindi au matokeo. Jioni hii vituo vya kupigia kura vitazungumza, hii itaakisi chaguo la Wasenegali. Tunatumai kuwa chaguo hili litakuwa bora zaidi kwa Senegal,” alihitimisha Rais Macky Sall, ambaye si mgombea wa nafasi yake mwenyewe.

    Kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko, ambaye sio mgomea wa urais alipiga kura katika ngome yake huko Ziguinchor (kusini) kabla ya kuzungumza na wanahabari.

    "Tunaona mmiminiko mkubwa wa Wasenegal kutoka nje na kutoka ndani ya nchi. Ninaamini hatujawahi kuona watu wengi kama hao katika masaa ya kwanza ya upigaji kura. Sina shaka kwamba mgombea wetu Bassirou Diomaye Faye atachaguliwa kwa wingi, na katika duru ya kwanza.”

    "Ninaomba utulivu na ninamtaka Waziri wa Mambo ya Ndani kuchukua hatua zote ili kuhakikisha kuwa kura hiyo inamalizika kwa amani ," aliongeza.

  4. Bassirou Diomaye Faye amepiga kura hivi punde

    .

    Mgombea Bassirou Diomaye Faye amepiga kura katika mji aliozaliwa, Ndiaganiao.

    Alitoa wito wa amani baada ya miezi kadhaa ya mvutano wa kisiasa.

    Yeye ndiye mgombea wa muungano wa Diomaye kwa uchaguzi wa urais nchini Senegal.

  5. Vita vya Ukraine: Mji wa Kyiv washambuliwa na Urusi

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Ukraine inasema imedungua makombora 18 ya Urusi na ndege zisizo na rubani 25 wakati wa shambulio kubwa katika mji mkuu.

    Wakazi walijificha katika vituo vya treni shambulio hilo lilipoanza saa 05:00 (03:00 GMT). Kulikuwa na uharibifu mdogo tu, maafisa wa Kyiv walisema.

    Takriban makombora 20 na ndege zisizo na rubani saba zililenga "miundombinu muhimu" katika eneo la magharibi la Lviv.

    Moja ya makombora ya cruise liliingia katika anga ya nchi jirani ya Poland, mwanachama wa Nato, vikosi vya silaha vilitangaza.

    "Kitu hicho kiliingia katika anga ya Poland karibu na mji wa Oserdow na kukaa huko kwa sekunde 39. Wakati kilipokuwa kikiruka kiliangaziwa na mifumo ya rada ya kijeshi," vikosi vilisema katika taarifa.

    Gavana aliyewekwa na Urusi wa bandari ya Sevastopol, iliyoko Crimea, alisema vikosi vya Urusi vilidungua makombora 10 ya Ukraine juu ya mji huo mwishoni mwa Jumamosi.

    Jengo la ofisi na njia ya gesi viliharibiwa na mwanamke akapata jeraha la misumari, Mikhail Razvozhayev alisema kwenye Telegraph.

    Siku ya Ijumaa, Urusi ilirusha makumi ya makombora dhidi ya Ukraine, na kugonga bwawa na kuwaacha raia milioni moja wa Ukraine bila nguvu za umeme.

  6. Watu wajificha huku wapiganaji wakiingia kwenye jumba la tamasha la Moscow

    Maelezo ya video, Watu wajificha huku wapiganaji wakiingia kwenye jumba la tamasha la Moscow
  7. Uchaguzi wa Senegal: Wapiga kura wachagua rais mpya baada ya mzozo wa kisiasa

    .
    Maelezo ya picha, Milolongo mirefu ya wapiga kura imeshuhudiwa nchi Senegal mapema leo

    Baada ya wiki kadhaa za machafuko ya kisiasa, watu nchini Senegal wanampigia kura rais mpya.

    Wagombea 17 wako kwenye kura, kila mmoja akitumai kuchukua nafasi ya Rais Macky Sall ambaye amezuiwa kuwania tena baada ya kufikisha kikomo cha mihula miwili.

    Uchaguzi huo ulikuwa ufanyike mwezi uliopita lakini Bw Sall aliahirisha, na kusababisha maandamano mabaya ya upinzani na mzozo wa kidemokrasia.

    Senegal hadi wakati huo ilisifiwa kama ngome ya demokrasia katika Afrika Magharibi.

    Watu milioni saba wanastahili kupiga kura katika uchaguzi wa Jumapili.

    Miongoni mwa wagombea wakuu ni mgombea wa muungano wa BBY, Waziri Mkuu wa zamani Amadou Ba, 62.

    Mpinzani wake mkubwa anaonekana kama Bassirou Diomaye Faye, 44, ambaye aliachiliwa kutoka jela wiki iliyopita tu, baada ya kuzuiliwa tangu Aprili 2023 kwa mashtaka ya uasi, ambayo alisema yalichochewa kisiasa.

    .
    Maelezo ya picha, Wapiga kura nchini Senegal
  8. Tazama video inayowaonesha wapiganaji ndani ya ukumbi wa Crocus Urusi

    Maelezo ya video, Video inayowaonesha wapiganaji ndani ya ukumbi wa Crocus Urusi

    Watu kadhaa wameuawa na kujeruhiwa wakati wa shambulio kwenye ukumbi wa tamasha karibu na mji mkuu wa Urusi Moscow, vyombo vya habari vya Urusi vinasema.

    Kanda za video zinaonyesha watu wenye bunduki kwenye ukumbi wa tamasha.

  9. Utekaji nyara wa Kuriga: Zaidi ya wanafunzi 280 wa Nigeria waachiliwa

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Magenge ya utekaji nyara yamekumba sehemu kubwa ya nchi katika miaka ya hivi karibuni, haswa kaskazini-magharibi

    Zaidi ya wanafunzi 280 wa Nigeria waliotekwa nyara katika mji wa kaskazini-magharibi wa Kuriga mapema mwezi huu wameachiliwa "bila kujeruhiwa", maafisa wanasema.

    Gavana wa jimbo la Kaduna Uba Sani hakutoa maelezo ya kuachiliwa kwao siku chache kabla ya tarehe ya mwisho ya kukombolewa iliyodaiwa na watekaji nyara.

    Watoto hao, wenye umri wa miaka minane hadi 15, na mwalimu mmoja, walitekwa nyara tarehe 7 Machi.

    Magenge ya utekaji nyara, yanayojulikana kama majambazi, yamekamata maelfu ya watu katika miaka ya hivi karibuni, haswa kaskazini-magharibi.

    Hata hivyo, kumekuwa na kupungua kwa utekaji nyara mkubwa wa watoto katika mwaka uliopita hadi wiki hii.

  10. Zelensky: Putin alikuwa kimya kwa siku - akifikiria jinsi ya kuiwekea lawama Ukraine

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Rais Zelensky

    Akizungumzia shambulio hilo katika Ukumbi wa Jiji la Crocus, Rais wa Ukraine Vladimir Zelensky alisema kwamba Vladimir Putin anajaribu kubadilisha uwajibikaji kwa kile kilichotokea kwa "mtu mwingine."

    "Siku zote wana mbinu sawa. Ilifanyika kabla. Na kulikuwa na nyumba zilizolipuliwa [huko Moscow na Ryazan mnamo 1999 - Ed.] na mauaji na milipuko. Na kila wakati wanalaumu wengine, "Zelensky alibainisha.

    "Jana haya yote yalitokea, na Putin, badala ya kushughulika na raia wake wa Urusi, kuwahutubia, alikaa kimya kwa siku - alifikiria jinsi ya kuilaumu Ukraine. Kila kitu kinatabirika kabisa, "Zelensky aliendelea.

    Kulingana na Zelensky, "ikiwa Warusi wako tayari kufa kimya kwenye crocuses na wasiulize maswali yoyote kwa huduma zao maalum, basi Putin atajaribu kugeuza zaidi ya hali moja kama hiyo kwa niaba ya nguvu yake ya kibinafsi."

  11. Idadi ya waliofariki kutokana na shambulio la ukumbi wa Crocus wafikia 133

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema watu wote wanne wenye silaha waliotekeleza shambulio baya katika eneo la tamasha lililojaa watu mjini Moscow wamekamatwa.

    Takriban watu 133 waliuawa na wengine zaidi ya 140 kujeruhiwa wakati washambuliaji walipovamia jengo hilo na kufyatua risasi kiholela na kuliteketeza.

    Mamlaka ilisema watu 11 walizuiliwa kwa jumla, na watu hao wanne wenye silaha walikamatwa wakielekea Ukraine.

    Kundi la Islamic State (IS) linasema ndilo lililohusika na shambulio hilo.

  12. Kundi la Islamic State ladai kuhusika na shambulio la ukumbi wa Croco Urusi

    .

    Chanzo cha picha, STRINGER/AFP

    Siku ya Ijumaa jioni, watu kadhaa waliojificha walifyatua risasi katika ukumbi wa tamasha wa Crocus City Hall huko Krasnogorsk karibu na Moscow, na kuua zaidi ya watu 130, wakiwemo watoto. Jioni hiyo hiyo, kundi la Islamic State, lilidai kuhusika na shambulio hilo.

    Upande wa Urusi bado haujatoa matoleo rasmi ya nani anaweza kuhusika. Idhaa za propaganda za Urusi ziliandika kwamba taarifa ya IS ilikuwa ya uwongo na ilidokeza kuhusika kwa Ukraine, ambayo inakanusha kabisa hili.

    Katika siku moja tangu shambulio hilo, IS ilitoa taarifa mpya, ambayo kwa mara nyingine ilieleza wajibu wake kwa kile kilichotokea katika Ukumbi wa Jiji la Crocus.

    Ripoti kutoka kwa shirika la habari la Amak, linaloaminika kuhusishwa na IS, ilichapisha picha inayoaminika kuwaonyesha washiriki wanne katika shambulio hilo. Katika picha, nyuso zao zimefunikwa nusu .

    Hata hivyo, kwa mujibu wa Mina Al-Lami, mtaalamu wa BBC kuhusu makundi yenye itikadi kali, ujumbe huu hautaji ni ofisi gani ya tawi la IS iliyotayarisha na kutekeleza shambulio hilo.

    Kulingana na Mina Al-Lami, kutotajwa kwa tawi la kikanda ni jambo la kawaida kwa IS.

  13. Natumai hujambo